Samsung: Kiwanda chetu hakina madhara ya kikemikali

Samsung imesema kufichua taarifa kama hizo ni kutoa siri za kibiashara.
Maelezo ya picha,

Samsung imesema kufichua taarifa kama hizo ni kutoa siri za kibiashara.

Kampuni ya kielektroniki ya Samsung ya Korea Kusini, imekanusha taarifa zilizotolewa na familia ambazo zinataka fidia ya madhara ya viwanda.

Kundi la wafanyakazi limesema watu 76 wamefariki kutokana na kemikali za kiwanda ambacho kinatengeneza bidhaa za samsung.

Maelezo ya picha,

Mamlaka inataka kujua aina ya kemikali inayotumika

Baadhi ya kesi zilimalizika lakini nyingine zinachelewa kutokana na mamlaka Kutaka kujua ni kemikali gani zimesababisha ugonjwa na vifo.

Samsung imesema kufichua taarifa kama hizo ni kutoa siri za kibiashara.

Imekanusha kuzuia taarifa kinyume na sheria.