UN kuchunguza mauaji Oromia na Amharia Ethiopia

Ramani ya Ethiopia
Umoja wa mataifa unataka Ethiopia kuruhusu waangalizi wa kimataifa kuingia katika maeneo ambayo hivi majuzi yaliathirika na maandamano yenye ghasia nchini humo.
Mkuu wa shirika la haki za binadamu laumoja wa mataifa Zeid Ra'ad Al Hussein anasema hakujakuwa na jaribio la kuchunguza ghasia hizo au kumpata mhusika.
Chanzo cha picha, AFP
Maelfu ya watu waliandamana dhidi ya sera ya serikali kuwapokonya ardhi
Shirika la haki za binadamu la kimataifa Amnesty International linasema kuwa takriban watu 100 waliuawa kwenye maandamano katika maeneo ya Oromia na Amhara mwishoni mwa wiki.
Waethiopia wazika waliouawa katika maandamano
Jumapili ilishuhudia makabiliano makali baina ya waandamanaji na maafisa wa utawala.
Waandamanaji hao walikuwa wakipinga sera mpya ya serikali ya kupanua jiji la Addis Ababa ambayo ililazimu baadhi yao kupokonywa ardhi.
Kulishuhudiwa pia maandamano makubwa katika eneo la Oromia ambako kunaaminika kuwa watu kadhaa waliuawa.

Waandamanaji 100 waliuawa Ethiopia- Amnesty
Waethiopia '100 waliuawa' kufuatia machafuko yaliyotokea wikiendi iliyopita polisi walipokabiliana na waandamanaji wa Oromia na Amharia Amnesty International inasema.