Afrika kwa Picha: 5 - 11 Agosti 2016

Huu hapa ni mkusanyiko wa picha za matukio muhimu barani Afrika, na picha za Waafrika kutoka maeneo mengine ulimwenguni, wiki hii.

Yemi Geoffrey Apithy (katikati) abeba bendera ya Benin katika uwanja wa Maracana, wakati wa ufunguzi wa michezo ya olimpiki mjini Rio de Janeiro, Brazil, Ijumaa.

Chanzo cha picha, EPA

Maelezo ya picha,

Yemi Geoffrey Apithy (katikati) abeba bendera ya Benin katika uwanja wa Maracana, wakati wa ufunguzi wa michezo ya olimpiki mjini Rio de Janeiro, Brazil, Ijumaa.

Chanzo cha picha, Reuters

Maelezo ya picha,

Bondia wa Cameroon Wilfred Seyi Ntsengue, asherehekea ushindi wake katika kitengo cha uzani wa kati (kilo 75) kwa wanaume, Jumanne.

Chanzo cha picha, Reuters

Maelezo ya picha,

Chuma yamzidi nguvu! Raia wa Cameroon Sonkbou Foudji akishiriki michezo ya kunyanyua vyuma, katika kitengo cha uzani wa kilo 69 kwa wanawake.

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha,

Wachezaji wa timu ya Kenya ya raga kwa watu saba kila upande washerehekea pamoja na mashabiki, hata baada ya kushindwa na Japan, 31-7, katika Olimpiki mjini Rio, uwanja wa Deodoro.

Chanzo cha picha, AP

Maelezo ya picha,

Tabasamu Rio! Msichana mdogo, shabiki wa timu ya voliboli ya Cameroon atabasamu kabla ya mechi ya ufunguzi kati ya Cameroon na Japan kwa wanawake siku ya Jumatatu.

Chanzo cha picha, EPA

Maelezo ya picha,

Alexandre Bouzaid raia wa Senegal aanguka wakati wa mchuano wa vitara dhidi ya raia wa Hungury siku ya Jumatano. Hatimaye Alexandre alishindwa na Boczko Gabor wa Hungury kwa pointi 15-9.

Chanzo cha picha, EPA

Maelezo ya picha,

Kutoka Rio, hadi Zimbabwe. Mwanajeshi aongoza wanajeshi wengine wakati wa maadhimisho ya siku ya wanajeshi wa Zimbabwe siku ya Jumatano, mbele ya rais wa taifa hilo Robert Mugabe.

Chanzo cha picha, Reuters

Maelezo ya picha,

Wafuasi wa rasi wa Zambia Edgar Lungu, na chama chake cha PF wawasili mjini Lusaka, kuhudhuria mkutano wa kisiasa kabla ya uchaguzi mkuu siku ya Jumatano.

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha,

Mwaniaji wa urais wa chama kikuu cha upinzani, Hakainde Hichilema pia alifanya mkutano wake wa mwisho mjini Lusaka siku iyo hiyo. Ushindani mkali unatarajiwa kati ya rais Edgar Lungu, na Hakainde Hichilema.

Chanzo cha picha, Reuters

Maelezo ya picha,

Zoezi la uchaguzi lilikuwa la amani na watu wengi walishiriki. Raia wa Zambia walipiga kura tano - ya urais, wabunge, mameya, madiwani na ya marekebisho ya kitengo cha haki za binadam kwenye katiba ya taifa hilo.