Mafuriko yasababisha vifo kaskazini mwa India

Mafuriko katika jimbo la Bihar

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha,

Mafuriko katika jimbo la Bihar

Mafuriko makubwa yaliyokumba eneo la kaskazini na kati ya India yamesababisha vifo vya zaidi ya watu mia moja hamsini.

Kwa mujibu wa serikali watu wengine milioni mbili nukta nne wameathiriwa katika jimbo la Bihar na miji mingine ya mashariki huku viwango vya maji katika mto Ganges vikizidi kuongezeka.

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha,

Watu watafuta makao Bihar

Maelfu ya watu wamepewa hifadi katika kambi lakini wengine hawataki kuondoka majumbani mwao.

Shirika la misaada la ActionAid limesema kumekuwa na uharibifu mkubwa hasa katika mashamba ya mpunga ambao huenda kukasababisha upungufu wa chakula.