Al Mahdi kuhukumiwa mahakama ya ICC

Al Mahdi kuhukumiwa mahakama ya ICC

Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu wa Kivita (ICC) inatarajiwa kutoa hukumu dhidi ya mwanamgambo wa Kiislamu raia wa Mali Ahmad Al Faqi Al Mahdi.

Al-Mahdi ameshtakiwa makosa ya uhalifu wa kivita kuhusiana na kuharibiwa kwa makaburi tisa na msikiti mashuhuri katika mji wa kale wa Timbuktu, 2012.