Wasanii Sudan kusini wachora kushinikiza amani Juba

Baada ya vita vya takriban miaka mitatu, wasanii Sudan kusini wameshirikiana katika kujaribu kuishinikiza nchi kukaa pamoja na kujadili amani, kwa kuanzisha michoro katika maeneo ya umma mjini Juba.

Kuta na mabohari yamechorwa kote mjini

Chanzo cha picha, Ana Taban

Maelezo ya picha,

Kuta na mabohari yamechorwa kote mjini

Mkusanyiko wa michoro ya Ana Taban (kutoka neno la kiarabu "nimechoka") linatokana na jina la vuguvugu la kuunga amani mkono Syria.

Chanzo cha picha, Ana Taban

Maelezo ya picha,

Mkusanyiko wa michoro ya Ana Taban (kutoka neno la kiarabu "nimechoka") linatokana na jina la vuguvugu la kuunga amani mkono Syria.

Michoro hiyo inaangazia mateso ya watoto katika vita vya kiraia. "mwishowe wao ndio watakaolazimika kukusanya kilichosalia na kuunganisha upya Sudan kusini," kundi hilo linasema.

Chanzo cha picha, Ana Taban

Maelezo ya picha,

Michoro hiyo inaangazia mateso ya watoto katika vita vya kiraia. "mwishowe wao ndio watakaolazimika kukusanya kilichosalia na kuunganisha upya Sudan kusini," kundi hilo linasema.

Kuta za shule taasisi za kitamaduni Juba zimepambwa kwa michoro ya wasanii hao.

Chanzo cha picha, Ana Taban

Maelezo ya picha,

Kuta za shule taasisi za kitamaduni Juba zimepambwa kwa michoro ya wasanii hao.

6

Chanzo cha picha, Ana Taban

Takriban watoto milioni moja wameachwa bila makaazi , jambo lililoliharibu taifa ambalo lilikuwa na matumaini makubwa wakati wa uhuru wake miaka itano iliyopita, lilipokuwa taifa changa duniani.

Chanzo cha picha, Ana Taban

Maelezo ya picha,

Takriban watoto milioni moja wameachwa bila makaazi , jambo lililoliharibu taifa ambalo lilikuwa na matumaini makubwa wakati wa uhuru wake miaka itano iliyopita, lilipokuwa taifa changa duniani.

Mojawapo ya wasanii

Chanzo cha picha, Ana Taban

Maelezo ya picha,

Abul Oyay Deng ni mwanafunzi aliyetoroka vita mnamo 2013, na kuishia Nairobi, lakini amerudi nyumbani kujiunga na mradi huo.

Wasanii hao wameshirikiana na wakaazi wa mitaa ya karibu katika baadhi ya michoro.

Chanzo cha picha, Ana Taban

Maelezo ya picha,

Wasanii hao wameshirikiana na wakaazi wa mitaa ya karibu katika baadhi ya michoro.

Mwanamume aliyechorwa akionekana anamtibu mtoto ni mfano wa Dr. Ding Col Dau, alierudi Sudan kusini mnamo 2014 kutoa huduma ya afya lakini aliuawa nyumbani kwake mwaka uliofuata.

Chanzo cha picha, Ana Taban

Maelezo ya picha,

Mwanamume aliyechorwa akionekana anamtibu mtoto ni mfano wa Dr. Ding Col Dau, alierudi Sudan kusini mnamo 2014 kutoa huduma ya afya lakini aliuawa nyumbani kwake mwaka uliofuata.

Tunakata mizizi yetu, tunajiangamiza - inangazia taswira ya mizozo inavyoharibuna kuathiri jamii.

Chanzo cha picha, Ana Taban

Maelezo ya picha,

Tunakata mizizi yetu, tunajiangamiza - inangazia taswira ya mizozo inavyoharibuna kuathiri jamii.

Kampeni ya kwenye mtandao #SaveTheLastTrain na mshairi Akol Miyen, ndiyo ilishinikiza mchoro huu. "Hii ndio treni ya mwisho kwasababu nafasi yetu kama taifa zinamalizika," kundi hilo linasema.

Chanzo cha picha, Ana Taban

Maelezo ya picha,

Kampeni ya kwenye mtandao #SaveTheLastTrain na mshairi Akol Miyen, ndiyo ilishinikiza mchoro huu. "Hii ndio treni ya mwisho kwasababu nafasi yetu kama taifa zinamalizika," kundi hilo linasema.

Baada ya kusambaza ujumbe wake katika baadhi ya kuta za mji wa Juba, kundi hilo sasa linapanga kupanua mradi wake nje ya mji mkuu huo.