Biden atokwa na machozi akipewa medali na Obama
Biden atokwa na machozi akipewa medali na Obama
Rais wa Marekani Barack Obama amemtunuku makamu wake Joe Biden Medali ya Rais ya Uhuru, ambayo ndiyo nishani ya hadhi ya juu zaidi anayoweza kupewa raia nchini Marekani.
Biden, ambaye alionekana kushangazwa na hatua hiyo, alitokwa na machozi alipokuwa anatunukiwa medali hiyo.

Mara saba Barack Obama alipotokwa na machozi
Rais wa Marekani anayeondoka Barack Obama alitokwa na machozi alipokuwa akitoa hotuba yake ya mwisho rasmi kama rais mjini Chicago.