Kifo mtoto Pendo kilivyofichua ukatili wakati wa maandamano Kenya
Kifo mtoto Pendo kilivyofichua ukatili wakati wa maandamano Kenya
Makundi ya kutetea haki za binadamu, yanasema idadi kubwa ya watu waliuawa na mamia zaidi kujeruhiwa katika ngome ya kiongozi wa upinzani Raila Odinga wakati wa maandamano yaliyotokea baada ya kutangazwa kwa matokeo ya uchaguzi wa urais wiki iliyopita.
Kisa kilichowagusa wengi ni kifo cha mtoto mwenye umri wa miezi sita Samantha Pendo, ambaye ambaye anadaiwa kupigwa na polisi mjini Kisumu, Magharibi mwa Kenya.
Mwandishi wa BBC Emmanuel Igunza anaarifu zaidi.