BBC yazindua Tuzo ya Komla Dumor ya 2018
BBC yazindua Tuzo ya Komla Dumor ya 2018
Shirika la utangazaji la Uingereza BBC limeanza tena mchakato wa kumtafuta nyota mpya wa uandishi kuhusu Afrika ambaye atatunukiwa Tuzo ya BBC ya Komla Dumor mwaka huu.
Huu utakuwa mwaka wa nne kwa tuzo hiyo kutolewa.
Wanahabari kutoka kote barani Afrika wanaombwa kuwasilisha maombi ya kushindania tuzo hii, ambayo hulenga kufichua na kuendeleza waandishi wapya wenye vipaji kutoka Afrika.