Hadhara Charles Mnjeja: Mwanadada aliyemvutia Trump kwa ustadi wake wa kupepeta mpira
Hadhara Charles Mnjeja: Mwanadada aliyemvutia Trump kwa ustadi wake wa kupepeta mpira
Video fupi inayomuonesha mwanadada Hadhara Charles Mnjeja kutoka Tanzania, akipepeta mpira kwa ustadi imepata umaarufu mkubwa katika mitandao ya kijamii.
Rais wa Marekani Donald Trump alitambua kazi ya Hadhara na kuandika katika mtandao wake wa Twitter kuwa ni kipaji kinacho stahili kukuzwa.
Mchezaji huyo wa miaka 29 yuko nchini Malawi hadi mwezi Machi ambako anajipatia riziki kupitia onyesho lake kupepeta mpira mitaani.
Analipisha dola tano kwa dakika mbili. Je anasemaje baada ya kutambuliwa na Trump?
"Nashukuru kuwa rais Trump anajua jina langu. Hatahivyo namuomba anisaidie kukuza kipaji changu kiwe baishara imara."

Video, Simba na Yanga: 'Nilizimia baada ya kumuweka mke rehani kwa shabiki wa Simba', Muda 1,15
Jimmy Kindoki ni shabiki wa sugu wa klabu ya Yanga ya Tanzania, lakini mapenzi kwa klabu yake nusura yamtokee puani wikendi.