'Wazazi waliponiambia niolewe niliamua kuwa DJ'

Wanawake ma DJ bado ni wachache katika ulimwengu wa muziki>mpiga picha wa BBC Photographer Sayan Hazra alifuatilia maisha ya DJ Puja Seth kazini, mmoja wa wanawake wachache wanaopiga disko kusini mwa Bangalore.
"Ninapenda kuwaona watu wakiupenda muziki wangu. Kwangu mimi, ni aina fulani ya uhuru, - hunifanya nijieleze kwa dunia,"anasema Bi Seth mwenye umri wa miaka 31.
- A.Kusini: Mbunge mwanamke ajitetea kwa kurusha ngumi
- Mauaji ya Khashoggi: Mwanamfalme wa Saudia kuchunguzwa
Alianza UDJ- mwaka 2014 Bangalore, mji ambao kwa kawaida unafahamika kama ''mji wa kumbi za muziki na baa'' kwa kuwa na utamaduni wa kumbi za muziki na vilabu vya pombe . Kwa miaka mingi , baa na kumbi za muziki zenye vilabu vya pombe, na vilabu vya pombe vimepanuliwa hadi nje ya kati kati mwa jiji ,na kufika hadi maeneo ya zamani, hata maeneo ya makazi ya watu.

"Nilipoanza kucheza miziki yangu kwenye vilabu ,, nilikutana na maDJ wanawake ambao walikuwa wakitembelea Bangalore kutoka miji mingine duniani - lakini nilivyoelewa mimi hakuna hata DJ mmoja mwanamke aliyekuwa anafanya kazi hii Bangalore."
Aliongeza kuwa, baada ya kupiga miziki mara chache alifahamika kama ''DJ mzawa mwanamke''

Lakini safari yake haikuwa rahisi. Akiwa ni mzaliwa wa kijiji cha mashariki mwa India kutoka kwa wazazi walioshikilia itikadi zao , Bi Seth anasema wakati wote amekuwa akitaka kufanya kazi ya kama DJ.
"Wazazi wangu wamemuwa kila mara niolewe-lakini sikutaka kufanya hilo."

Mara alipomaliza shule ya sekondari, alimua kutoroka kwao na "kufuata ndoto yake".
"Katika jamii yangu, wanawake hawaruhusiwi kufanya kazi - na wengi wao hawatoki nyumbani kwao peke yao hadi watakapoolewa. Kwa hiyo nilifahamu fika nilazima niondoke."

Utafutaji wake wa kazi ulimpeleka hadi Bangalore ambako alianza kufanya kazi kama muhudumu wa ndege.
Hapo ndipo alipokwenda kwenye sherehe kwa mara ya kwanza.
"Kitu cha kwanza nilichokigundua alikuwa ni DJ na ninakumbuka nilivutiwa sana ,"alisema.
Baada ya hilo, alijua ni nini anachotaka kukifanya.

"Nilijenga urafiki na baadhi ya maD mjini ambao walinifundisha ujuzi wa kimsingi wa DJ. mengine nilijifunza kwa kutazama video za YouTube ."
Bi Seth amekwisha piga miziki yake katika matukio zaidi ya 450 kote nchini India kwa kipindi cha miaka mitano iliyopita.
- Kwa nini wanawake India wanazikataa chale
- Wanawake wasusia zawadi ya Sari India
- India yaongeza mara dufu likizo ya wanawake kujifungua
"Nilikuwa sijawahi kuwaona wanawake wakinywa pombe na kuvuta sigara katika kijiji changu - na sasa ninaupigia muziki umati wa watu ambao wanafanya yote hayo karibu yangu na sifungi macho."
Licha ya kupendeza , anasema, kuwa DJ-kama mwanamke ina hatari zake: "Watu husema mara kwa mara kuwa taaluma hii si ya wanawake."

"Katika vilabu vya pombe watu wanalewa, na nadhani wanaweza kunifuata kila mara. Mara nyingi, huwa wananiomba namba yangu ya simu. Na wakati mwingine, ni vigumu kuwapuuza na kufanya kazi yangu - lakini huwa ninapata usaidizi kutoka kwa walinzi(mabaunsa)."
Lakini hajakubali hayo yamzuwie kufanya kazi yake.
"Kitu kizuri zaidi kuhusu kazi yangu ni kuifanya hadhira i densi , kuwaona wakiuhisi muziki kama mimi. Watu huja katika muziki wangu kwa ajili ya kupata hisia hiyo ."
Picha zote na Sayan Hazra