Got a TV Licence?

You need one to watch live TV on any channel or device, and BBC programmes on iPlayer. It’s the law.

Find out more
I don’t have a TV Licence.

Habari za moja kwa moja

time_stated_uk

  1. Magufuli alivyopokelewa na Kenyatta ikulu Nairobi

    Maafisa wa Rais Uhuru Kenyatta, kwenye akaunti yake ya Twitter, wamepakia picha za jinsi Rais wa Tanzania John Magufuli alivyolakiwa ikulu, Nairobi.

    Rais Magufuli akikagua gwaride la heshima
    Image caption: Rais Magufuli akikagua gwaride la heshima
    Rais Magufuli na Rais Kenyatta
    Image caption: Rais Magufuli na Rais Kenyatta
    Rais Kenyatta, Rais Magufuli na mkuu wa majeshi wa Kenya Jenerali Samson Mwathethe
    Image caption: Rais Kenyatta, Rais Magufuli na mkuu wa majeshi wa Kenya Jenerali Samson Mwathethe
    Rais Kenyatta na Rais Magufuli wakiwa ikulu, Nairobi.
    Image caption: Rais Kenyatta na Rais Magufuli wakiwa ikulu, Nairobi.
  2. Magufuli: Kenya ni mshirika wetu mkubwa Afrika

    Magufuli: Kenya ni mshirika wetu mkubwa kibiashara Afrika

    Rais wa Tanzania John Pombe Magufuli amesema kuwa Kenya ndio mshirika nambari moja wa Tanzania katika uwekezaji na biashara barani Afrika.

    Akizungumza katika ikulu ya rais jijini Nairobi mda mfupi baada ya kuwasili nchini Kenya,Rais Magufuli amesisitiza kuwa hakuna taifa jingine ambalo limewekeza nchini mwake kama Kenya.

    Amesema kuwa kulingana na rekodi za uwekezaji nchini Tanzania kuna takriban kampuni 529 nchini humo kutoka Kenya ambazo zinaingiza takriban dola bilioni 1.7 kila mwaka huku takriban Watanzania 57,260 wakiwa wameajiriwa.

    Rais huyo vilevile ametoa wito kwa Wakenya wanaotaka kuwekeza nchini Tanzania kuharakisha hatua hiyo.

    Aidha ameongezea kuwa amekuwa akiwasiliana na rais Uhuru Kenyatta mara kwa mara na kiwakosoa wale wanaodhani kwamba uhusiano wake na rais wa Kenya una utata.

    Rais John Pombe Magufuli na mwenzake wa Kenya Uhuru Kenyatta baada ya kiongozi huyo wa Tanzania kuwasili nchini Kenyai
  3. Magufuli alakiwa na waziri wa mambo ya nje

    Wizara ya mambo ya nje Kenya imepakia picha za Rais Magufulia kilakiwa uwanja wa ndege na waziri wa mambo ya nje wa Kenya Bi Amina Mohamed. Bi Mohamed anawania wadhifa wa rais wa tume ya Umoja wa Afrika (AU).

    Magufuli awasili Kenya
    Rais Magufuli akipatiwa shada la maua na mshichana uwanja wa ndege
    Image caption: Rais Magufuli akipatiwa shada la maua na mshichana uwanja wa ndege
    Rais Magufuli na Bi Amina Mohamed
    Image caption: Rais Magufuli na Bi Amina Mohamed
    Magufuli akitia saini kitabu cha wageni
    Image caption: Magufuli akitia saini kitabu cha wageni
  4. Kenya inataka nini ziara ya Magufuli?

    Msemaji wa Rais Kenyatta, Manoah Esipisu, Jumapili aligusia baadhi ya mambo ambayo Kenya inatarajia kutoka kwa ziara ya Rais Magufuli nchini Kenya.

    Alisema: “Ziara ya Rais huyu inatupatia fursa ya kufanya upya na kukoleza uhusiano wetu katika nyanja mbalimbali. Viongozi wa nchi hizi watashauriana kuhusu masuala mbalimbali ya pamoja katika ngazi ya taifa kwa taifa na kanda. Wataangazia sana masuala ambayo tayari kumekuwa na mazungumzo, na tunatarajia matokeo ya mazungumzo hayo kutangazwa.

    “Masuala kadha yatajadiliwa, ikiwemo ada ya vibali vya kufanyia kazi ambayo raia wa Kenya hutozwa, pamoja na karo ya juu ambayo Wakenya hutozwa vyuo vikuu (Tanzania). Mashauriano kuhusu kuondoa vikwazo vya kibiashara baina ya nchi hizi mbili pia yatafanyika. Kadhalika, na muhimu sana katika mazungumzo hayo ni shughuli za magari ya kusafirisha watalii yanayovuka mipaka.

    “Muhimu katika mashauriano haya itakuwa pia kufufuliwa kwa Tume ya Ushirikiano wa Pamoja na Tanzania (JCC) ambayo ni jukwaa ambalo linaweza kutumiwa kutangaza biashara na uwekezaji  baina ya nchi zote mbili.

    “Rais Kenyatta  pia atazungumza na Rais Magufuli kumhusu Bi Amina Mohammed (waziri wa mambo ya nje wa Kenya) anayewania wadhifa wa mwenyekiti wa Tume ya Umoja wa Afrika.

  5. Magufuli awasili ikulu, Nairobi

    Rais Magufuli amewasili katika ikulu ya Nairobi ambapo amekagua gwaride la heshima. Pia amepigiwa mizinga 21 kama ilivyo ada kwa viongozi wa mataifa wanapozuru Kenya.

  6. Mambo matano atakayoyafanya Magufuli akiwa Kenya

    Wakati wa ziara yake ya siku mbili Kenya Rais Magufuli, kwa mujibu wa ikulu ya Tanzania, anatarajiwa:

    1. Atafanya mazungumzo rasmi na mwenyeji wake Rais Uhuru Kenyatta
    2. Atatoa heshima katika Kaburi la Rais wa Kwanza wa Kenya Hayati Mzee Jomo Kenyatta.
    3. Atahudhuria dhifa ya kitaifa atakayoandaliwa na mwenyeji wake Ikulu Jijini  Nairobi.
    4. Atatembelea kiwanda cha maziwa cha  Eldoville kilichopo Karen Jijini Nairobi
    5. Atazindua barabara mchepuko (Southern By-pass) iliyopo jijini Nairobi.
    Magufuli uwanja wa JNIA
  7. Magufuli amewasili 'mapema'

    Mwandishi wa gazeti la kibinafsi la Nation, Kenya ameandika kwenye Twitter kwamba Rais Magufuli tayari amewasili uwanja wa ndege wa Jomo Kenyatta. Mwandishi huyo anasema huenda kiongozi huyo amewasili mapema kuliko ilivyotarajiwa.

  8. Ziara ya Magufuli kwa kibonzo

    Mchoraji vibonzo mashuhuri Afrika Mashariki, Godfrey Mwapembwa maarufu kama Gado amepakia kwenye Twitter kibonzo kuhusu ziara ya Rais Magufuli Kenya.

  9. Viongozi wamuaga Magufuli JNIA

    Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan akiwa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi,  Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda na viongozi wengine wakipunga mikono kumuaga Rais  Magufuli  katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere wakati akianza safari ya kwenda Nairobi.

    Viongozi wamuaga Magufuli
    Rais Magufuli akisindikizwa na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan katika Uwanja wa ndege.
    Image caption: Rais Magufuli akisindikizwa na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan katika Uwanja wa ndege.
  10. Magufuli aabiri ndege kwenda Kenya

    Ikulu ya Rais Tanzania imepakia picha hii mtandaoni, ya Rais Dkt John Pombe Magufuli akipunga mkono wakati akipanda ndege kwenye Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere tayari kwa safari ya kwenda Nairobi, Kenya. Ziara hiyo ni ya siku mbili.   

    Rais Magufuli akiabiri ndege kwenda Kenya
    Image caption: Rais Magufuli akiabiri ndege kwenda Kenya
  11. Rais Magufuli aanza ziara ya kwanza Kenya

    Magufuli kushauriana na Kenyatta na kuzindua barabara

    Rais wa Tanzania John Magufuli anatarajiwa kuanza ziara yake ya kikazi katika nchi jirani ya Kenya leo.

    Kwenye ziara hiyo ya siku mbili, Rais Magufuli anatarajiwa kufanya mazungumzo na mwenyeji wake na pia kuzindua barabara mchepuko ya Southern By-pass iliyopo Jijini Nairobi.

    Barabara hiyo, ambayo inaunganisha maeneo mbalimbali ya jiji la Nairobi kwa barabara za juu na chini, ni moja kati ya miradi mbalimbali ya ujenzi wa barabara ambayo imekuwa ikitekelezwa na serikali ya Kenya kupunguza msongamano wa magari katika jiji hilo kuu.

    Rais Magufuli na Rais Kenyatta