Na hapo ndio tunakamilisha matangazo ya moja kwa moja kwa hii leo. Asante kwa kusoma taarifa zetu.
Mke wa waziri mkuu nchini Israel akiuka kanuni za corona
EPACopyright: EPA
Sara Netanyahu amejitetea akisema, alidhani anaruhusiwa kutengenezwa nywele kwasababu ya kushiriki kwenye utengenezaji wa filamu ya kuhamasisha umma.Image caption: Sara Netanyahu amejitetea akisema, alidhani anaruhusiwa kutengenezwa nywele kwasababu ya kushiriki kwenye utengenezaji wa filamu ya kuhamasisha umma.
Ripoti zinadai kwamba mke
wa Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu, Sara, amevunja kanuni zilizowekwa za
kukabiliana na ugonjwa wa Covid-19 ili atengenezwe nywele.
Kulingana na gazeti la
Yedioth Ahronoth, msusi alikwenda kwenye makazi rasmi ya waziri mkuu wiki
iliyopita.
Hata hivyo, kanuni
zilizowekwa mwezi uliopita baada ya kuongezeka kwa idadi ya maambukizi ikiwemo
kutoruhusiwa kutembea zaidi ya kilomita 1 kutoka eneo lako la nyumbani
isipokuwa tu kwa mahitaji maalum.
Hayo hayajumuishi
mahitaji ya urembo kwa mtu ambaye hana majukumu rasmi kama mke wa Netanyahu.
Kutembelea makazi ya
mwingine pia hakuruhusiwi.
Vyanzo vinasema Bi. Netanyahau alijitetea akisema alifikiria
kwamba anaruhusiwa kutengenezwa nywele kwasababu alikuwa anashiriki utengenezaji wa filamu ya
kuhamasisha umma kuhusu umuhimu wa kuvaa barakoa.
Aidha, waliongeza kwamba yeye na msusi wake walivaa
barakoa na glavu wakati anatengenezwa nywele na pia alimuomba msusi wake
kuepuka kuzungumza.
Bi. Netanyahau, ndio wa hivi karibuni miongoni mwa watu
wa ngazi ya juu kuvunja kanuni za kukabiliana na virusi vya corona.
Janga laathiri ukuaji uchumi wa mwongo mmoja Afrika
Getty ImagesCopyright: Getty Images
Ukuaji wa uchumi huenda ukaimarika mwaka ujaoImage caption: Ukuaji wa uchumi huenda ukaimarika mwaka ujao
Benki ya Dunia imesema janga la virusi vya corona limeathiri
ukuaji wa uchumi Afrika na huenda kukasababisha kushuka kwa uchumi kwa asilimia
3.3 mwaka huu wa 2020.
Hata hivyo, benki hiyo inatabiri kuimarika kwa uchumi huo
mwaka ujao.
Hadi kufikia sasa, Afrika imefanikiwa kukwepa athari
kubwa za janga la corona huku idadi ya maambukizi ikiwa chini ikilinganishwa na
mabara mengine.
Lakini hatua ya kutotoka nje ili kukabiliana na janga
hilo kumesababisha ukuaji wa kasi ya chini ya uchumi, hususan Afrika Kusini
nchi ya pili yenye ukuaji mkubwa wa uchumi.
Benki wa Dunia imeonya kwamba raia zaidi ya milioni 40
huenda wakatumbukia kwenye lindi la umaskini.
'Sokwe azaliwa licha ya vipimo vya ujauzito wa mama yake kukutwa hana mimba’
CHESTER ZOOCopyright: CHESTER ZOO
Hifadhi ya wanyama ya Chris Yarwood imesema bado haijafahamu jinsia ya sokwe aliyezaliwaImage caption: Hifadhi ya wanyama ya Chris Yarwood imesema bado haijafahamu jinsia ya sokwe aliyezaliwa
Sokwe amezaliwa kiajabu katika
hifadhi ya wanyama baada ya mama yake kupimwa ujauzito miezi michache iliyopita
kabla hajajifungua na kukutwa hana mimba.
Mhudumu wa hifadhi hiyo ya wanyama
Chris Yarwood amesema sokwe huyo amezaliwa baada ya mama yake kufanyiwa vipimo
kadhaa na kukutwa hana ujauzito.
Ameongeza kuwa mtoto huyo wa sokwe
alizaliwa mwezi Juni, na alimficha kwa wahudumu tangu alipozaliwa.
Matokeo yake, wahudumu hawafahamu
jinsia ya sokwe huyo mpaka sasa.
Katika kisiwa cha Asia, sokwe wako hatarini
sana kupotea na sasa wamesalia 55,000.
CHESTER ZOOCopyright: CHESTER ZOO
Mama Leia amekuwa akimficha mtoto wake tangu alipozaliwa mwezi JuniImage caption: Mama Leia amekuwa akimficha mtoto wake tangu alipozaliwa mwezi Juni
Bwana Yarwood amesema kuzaliwa kwa
sokwe huyo mpya kumewapa matumaini mapya licha ya kwamba dunia haina uhakika wa
uwepo wao, lakini maisha yanaendelea kama kawaida na kuzaliwa kwa sokwe huyo kumetoa
mwangaza mpya".
Mtoto huyo wa sokwe ni wa pili kuzaliwa
kutokana na sehemu ya mpango wa njia ya kupandikiza wanyama katika hifadhi.
Awali hifadhi hiyo ya wanyama ilisema
programu za aina hiyo zimekumbana na changamoto ya ufadhili baada ya kutokea
kwa ugonjwa wa Covid 19.
Nzi atawala mdahalo wa makamu rais Marekani
BBCCopyright: BBC
Nzi aliyetawala mdahalo wa makamu wa rais MarekaniImage caption: Nzi aliyetawala mdahalo wa makamu wa rais Marekani
Ikiwa
moja ya vipimo vya mafanikio ni umaarufu kwenye mitandao ya kijamii basi
mdahalo wa makamu rais Marekani umechukua kikombe.
Licha ya wagombea hao
kujitahidi kwa kila namna kwenye hoja zao, hakuna walichosema kilichoendana na
watu waliokuwa wanawafuatilia mitandaoni kama ilivyokuwa kwa nzi aliyejitokeza
ambaye hakukutarajiwa.
Kwa takriban dakika
mbili, nzi alitua kwenye kichwa cha makamu rais Mike Pence na moja kwa moja
akawa maarufu.
Neno ‘nzi’ limesambaa
kwenye mtandao wa Twitter zaidi ya mara 700,000 tangu alipojiteokeza wakati mdahalo
unaendelea.
Kampeni ya Joe Biden
nayo imetumia vizuri fursa hiyo kwa kusambaza maneno "flywillvote.com".
Nzi huyo ameunganisha pande
zote mbili huku mmoja akimpachika jina la "shujaa wa Marekani" na
mwingine akisema "huenda ndio jambo litakalokumbukwa zaidi".
Aidha, mmoja amelinganisha wakati wa mdahalo wa urais
katika uchaguzi uliotanguliwa – miaka minne iliyopita ambapo nzi alijitokeza
juu ya kichwa cha mgombea urais Hillary Clinton.
Hilo halimaanishi kwamba nzi huyo ni yule yule aliyejitokeza
wakati huo na sasa amerejea tena.
Lakini sio wote waliomchukulia nzi huyo kwa utani kwasababu
mchambuzi mwenye msimamo mkali Ben Shapiro alisema kuwa nzi huyo ni njia moja
ya kutatiza kile kilichokuwa kinaendelea wakati wa mdahalo.
Viongozi wa Kenya na Misri wajadiliana juu ya mzozo wa mto Nile
State House KenyaCopyright: State House Kenya
Rais wa Misri Abdel Fattah al-Sisi (kulia) na rais wa Kenya Uhuru Kenyatta (kushoto)Image caption: Rais wa Misri Abdel Fattah al-Sisi (kulia) na rais wa Kenya Uhuru Kenyatta (kushoto)
Mkutano kati ya rais wa
Misri Abdel Fattah al-Sisi na rais wa Kenya Uhuru Kenyatta umengazia majadiliano yaliokwama
ya bwawa la Ethiopia, kulingana na maafisa wa Misri.
Viongozi hao wawili walikutana
katika mji mkuu wa Cairo, Jumapili wakati rais Kenyatta anarejea nyumbani
kutoka Ufaransa.
Taarifa kutoka kwa
msemaji wa Misri inasema: “Mkutano huo uligusia maendeleo ya hivi karibu yenye maslahi
ya mataifa hayo mawili, hasa yenye kuzingatia bwawa la Ethiopia, kama ilivyokubalika
kuimarisha uhusiano kati ya nchi hizo mbili wakati wa kipindi kijacho juu ya
suala hili nyeti na muhimu".
Kenya haikusema lolote kuhusu bwawa hilo zaidi ya kusema kuwa viongozi hao walijadiliana masuala
yenye kugusa maslahi ya nchi hizo mbili, miongoni mwao amani ya eneo na
usalama, biashara na namna Afrika inavyokabiliana na ugonjwa wa Covid-19.
Bwawa la Ethiopia
linalojengwa kutoka mto Nile linatarajiwa kutoa nguvu za umeme kwa raia milioni
65 wa Ethiopia.
Kwa kaisi kikubwa mno, Misri
inategemea mto Nile kwa maji ya matumizi yake na hivi karibuni ilionya kwamba
ujenzi wa bwawa hilo ni tishio kwa taifa lake.
Kenya ni mmoja wa waangalizi
katika jopo la wapatanishi la Umoja wa Afrika katika utatuzi wa mgogoro unatokana na
bwawa hilo.
Mali imemuachilia Waziri Mkuu wa zamani aliyekuwa amekamatwa
Mali imemuachilia Waziri
Mkuu wa zamani aliyekuwa amekamatwa.
Mamlaka huko Mali
imetangaza kuachiliwa huru kwa wanasiasa kadhaa na wanajeshi waliokamatwa
wakati wa mapinduzi ya Agosti.
Walioachiliwa ni pamoja
na aliyekuwa Waziri Mkuu, Boubou Cissé.
Taarifa rasmi
imeonesha kwamba waliokamatwa bado watasubiri uamuzi wa mahakama ikiwa kutakuwa
na haja ya kufanya hivyo.
Jumatatu, serikali ya
mpito ilitangaza baraza jipya la mawaziri ambapo wanajeshi waliopanga mapinduzi
walikabidhiwa nafasi muhimu serikalini ikiwemo ulinzi, usalama, utawala wa
mipaka na maridhiano ya kitaifa.
Jumuiya ya
Kiuchumi ya Nchi za Afrika Magharibi ECOWAS, imeiondolea Mali vikwazo, na
kutambua kile ilichokitaja kama kupigwa kwa hatua muhimu kuelekea kwenye
utaratibu wa kikatiba.
Getty ImagesCopyright: Getty Images
Boubou Cissé ni miongoni mwa walioachiliwa huruImage caption: Boubou Cissé ni miongoni mwa walioachiliwa huru
Nani ataingia kwenye fainali ya kuwania uongozi wa (WTO)
BBCCopyright: BBC
Wanaowania nafasi ya kuongoza WTOImage caption: Wanaowania nafasi ya kuongoza WTO
Wagombea
watano wanaowania kuchukua uongozi wa Shirika la Biashara Duniani (WTO),
wanatarajia kufahamu nani anaingia kwenye fainali ya kinyang’anyiro hicho,
Alhamisi.
Kumekuwa
na tetesi kwamba huenda wagombea wa Nigeria na Korea Kusini wakaingia kwenye
awamu ya fainali.
Aidha
Shirika la WTO halijawahi kuongozwa ama na mwanamke au mwafrika.
Wagombea
wote wamekuwa na majukumu wanayoyatekeleza katika ngazi ya kidunia.
Aliyekuwa
waziri wa fedha wa Nigeria Ngozi Okonjo-Iweala aliwahi kuhudumu kama Mkurugenzi
mkuu wa Benki ya Dunia ilihali akiwa waziri wa fedha wa Kenya, Amina Mohamed alikuwa
mwenyekiti wa mkutano wa mawaziri wa WTO katika mkutano uliofanyika Nairobi
mwaka 2015.
Aidha,
wawili hao wanakabiliwa na upinzani kutoka kwa waziri wa biashara wa Korea
Kusini Yoo Myung-hee, pamoja na Mohammad Maziad Al-Tuwaijri mshauri wa familia ya
kifalme wa Saudi Arabia na Liam Fox, aliyekuwa waziri wa Uingereza.
Matumaini
ni kwamba ikiwa mwafrika ndiye atakayechaguliwa kuongoza Shirika la WTO, hilo
huenda likaimarisha uchumi, ambao umekwama kwa asilimia 2 hadi 3 kwa muda
katika kiwango cha wastani duniani.
Mgombea
atakayeibuka na ushindi anatarajiwa kutangazwa mwezi ujao.
Joshua Cheptegei avunja rekodi ya mita 10,000
Getty ImagesCopyright: Getty Images
Cheptegei sasa anashikilia rekodi nne za duniaImage caption: Cheptegei sasa anashikilia rekodi nne za dunia
Mwanariadha wa Uganda Joshua
Cheptegei alivunja rekodi ya dunia upande wa wanaume katika mbio za mita 10,000
huku mwanariadha wa Ethiopia Letesenbet Giedy akivunja rekodi ya wanawake
katika mbio za mita 5000 mjini valencia nchini Uhispania.
Cheptegei mwenye umri
wa miaka 24 aliweka muda wa dakika 26 na sekunde 11 na kuvunja rekodi ya
miaka 15 iliowekwa na mwanariadha wa Ethiopia Kenenisa Bekele kwa zaidi ya
sekunde sita.
Getty ImagesCopyright: Getty Images
Gidey alivunja rekodi ya dunia ya miaka 12Image caption: Gidey alivunja rekodi ya dunia ya miaka 12
Gidey
mwenye umri wa miaka 22 aliweka muda wa dakika 14 na sekunde 6.62 na kuvunja
rekodi iliowekwa na Tirunesh Dibaba 2008.
Walifikia
muda huo katika mbioa za NN Valencia za rekodi za dunia.
Nafurahia
alisema Gidey ambaye alishinda medali ya shaba katika mbio za mita 10,000 kwenye
mashindano ya riadha ya dunia mjini Doha Qatar 2019.
‘’Hii
imekuwa ndoto ya muda mrefu. Ni kitu kikubwa kwangu. Rekodi ya Bekele ya awali
ya muda wa dakika 26 na sekunde 17 .53 ilisimama kwa muda mrefu bila
kuvunjwa’’.
Rekodi
ya awali ya Bekele ya dakika 26 na sekunde 17.53 ilikuwa ndio ya muda mrefu
zaidi kudumu katika historia kwa mbio za mita 10,000 kwa wanaume.
Mafanikio
ya Cheptegei yanaadhimisha rekodi ya nne duniani katika kipindi cha miezi 10,
baada ya kuvunja rekodi ya mbio za marathoni ya kilomita 10 Desemba na kilomita
5 mwezi Februari.
Katika
mbio za Monaco Diamond League zilizofanyika Agosti, alivunja rekodi nyingine ya
dunia ya Bekele, ya miaka 16 ya mita 5,000 kwa sekunde mbili.
Habari za moja kwa moja
Na Asha Juma
time_stated_uk
Na hapo ndio tunakamilisha matangazo ya moja kwa moja kwa hii leo. Asante kwa kusoma taarifa zetu.
Mke wa waziri mkuu nchini Israel akiuka kanuni za corona
Ripoti zinadai kwamba mke wa Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu, Sara, amevunja kanuni zilizowekwa za kukabiliana na ugonjwa wa Covid-19 ili atengenezwe nywele.
Kulingana na gazeti la Yedioth Ahronoth, msusi alikwenda kwenye makazi rasmi ya waziri mkuu wiki iliyopita.
Hata hivyo, kanuni zilizowekwa mwezi uliopita baada ya kuongezeka kwa idadi ya maambukizi ikiwemo kutoruhusiwa kutembea zaidi ya kilomita 1 kutoka eneo lako la nyumbani isipokuwa tu kwa mahitaji maalum.
Hayo hayajumuishi mahitaji ya urembo kwa mtu ambaye hana majukumu rasmi kama mke wa Netanyahu.
Kutembelea makazi ya mwingine pia hakuruhusiwi.
Vyanzo vinasema Bi. Netanyahau alijitetea akisema alifikiria kwamba anaruhusiwa kutengenezwa nywele kwasababu alikuwa anashiriki utengenezaji wa filamu ya kuhamasisha umma kuhusu umuhimu wa kuvaa barakoa.
Aidha, waliongeza kwamba yeye na msusi wake walivaa barakoa na glavu wakati anatengenezwa nywele na pia alimuomba msusi wake kuepuka kuzungumza.
Bi. Netanyahau, ndio wa hivi karibuni miongoni mwa watu wa ngazi ya juu kuvunja kanuni za kukabiliana na virusi vya corona.
Janga laathiri ukuaji uchumi wa mwongo mmoja Afrika
Benki ya Dunia imesema janga la virusi vya corona limeathiri ukuaji wa uchumi Afrika na huenda kukasababisha kushuka kwa uchumi kwa asilimia 3.3 mwaka huu wa 2020.
Hata hivyo, benki hiyo inatabiri kuimarika kwa uchumi huo mwaka ujao.
Hadi kufikia sasa, Afrika imefanikiwa kukwepa athari kubwa za janga la corona huku idadi ya maambukizi ikiwa chini ikilinganishwa na mabara mengine.
Lakini hatua ya kutotoka nje ili kukabiliana na janga hilo kumesababisha ukuaji wa kasi ya chini ya uchumi, hususan Afrika Kusini nchi ya pili yenye ukuaji mkubwa wa uchumi.
Benki wa Dunia imeonya kwamba raia zaidi ya milioni 40 huenda wakatumbukia kwenye lindi la umaskini.
'Sokwe azaliwa licha ya vipimo vya ujauzito wa mama yake kukutwa hana mimba’
Sokwe amezaliwa kiajabu katika hifadhi ya wanyama baada ya mama yake kupimwa ujauzito miezi michache iliyopita kabla hajajifungua na kukutwa hana mimba.
Mhudumu wa hifadhi hiyo ya wanyama Chris Yarwood amesema sokwe huyo amezaliwa baada ya mama yake kufanyiwa vipimo kadhaa na kukutwa hana ujauzito.
Ameongeza kuwa mtoto huyo wa sokwe alizaliwa mwezi Juni, na alimficha kwa wahudumu tangu alipozaliwa.
Matokeo yake, wahudumu hawafahamu jinsia ya sokwe huyo mpaka sasa.
Katika kisiwa cha Asia, sokwe wako hatarini sana kupotea na sasa wamesalia 55,000.
Bwana Yarwood amesema kuzaliwa kwa sokwe huyo mpya kumewapa matumaini mapya licha ya kwamba dunia haina uhakika wa uwepo wao, lakini maisha yanaendelea kama kawaida na kuzaliwa kwa sokwe huyo kumetoa mwangaza mpya".
Mtoto huyo wa sokwe ni wa pili kuzaliwa kutokana na sehemu ya mpango wa njia ya kupandikiza wanyama katika hifadhi.
Awali hifadhi hiyo ya wanyama ilisema programu za aina hiyo zimekumbana na changamoto ya ufadhili baada ya kutokea kwa ugonjwa wa Covid 19.
Nzi atawala mdahalo wa makamu rais Marekani
Ikiwa moja ya vipimo vya mafanikio ni umaarufu kwenye mitandao ya kijamii basi mdahalo wa makamu rais Marekani umechukua kikombe.
Licha ya wagombea hao kujitahidi kwa kila namna kwenye hoja zao, hakuna walichosema kilichoendana na watu waliokuwa wanawafuatilia mitandaoni kama ilivyokuwa kwa nzi aliyejitokeza ambaye hakukutarajiwa.
Kwa takriban dakika mbili, nzi alitua kwenye kichwa cha makamu rais Mike Pence na moja kwa moja akawa maarufu.
Neno ‘nzi’ limesambaa kwenye mtandao wa Twitter zaidi ya mara 700,000 tangu alipojiteokeza wakati mdahalo unaendelea.
Kampeni ya Joe Biden nayo imetumia vizuri fursa hiyo kwa kusambaza maneno "flywillvote.com".
Nzi huyo ameunganisha pande zote mbili huku mmoja akimpachika jina la "shujaa wa Marekani" na mwingine akisema "huenda ndio jambo litakalokumbukwa zaidi".
Aidha, mmoja amelinganisha wakati wa mdahalo wa urais katika uchaguzi uliotanguliwa – miaka minne iliyopita ambapo nzi alijitokeza juu ya kichwa cha mgombea urais Hillary Clinton.
Hilo halimaanishi kwamba nzi huyo ni yule yule aliyejitokeza wakati huo na sasa amerejea tena.
Lakini sio wote waliomchukulia nzi huyo kwa utani kwasababu mchambuzi mwenye msimamo mkali Ben Shapiro alisema kuwa nzi huyo ni njia moja ya kutatiza kile kilichokuwa kinaendelea wakati wa mdahalo.
Viongozi wa Kenya na Misri wajadiliana juu ya mzozo wa mto Nile
Mkutano kati ya rais wa Misri Abdel Fattah al-Sisi na rais wa Kenya Uhuru Kenyatta umengazia majadiliano yaliokwama ya bwawa la Ethiopia, kulingana na maafisa wa Misri.
Viongozi hao wawili walikutana katika mji mkuu wa Cairo, Jumapili wakati rais Kenyatta anarejea nyumbani kutoka Ufaransa.
Taarifa kutoka kwa msemaji wa Misri inasema: “Mkutano huo uligusia maendeleo ya hivi karibu yenye maslahi ya mataifa hayo mawili, hasa yenye kuzingatia bwawa la Ethiopia, kama ilivyokubalika kuimarisha uhusiano kati ya nchi hizo mbili wakati wa kipindi kijacho juu ya suala hili nyeti na muhimu".
Kenya haikusema lolote kuhusu bwawa hilo zaidi ya kusema kuwa viongozi hao walijadiliana masuala yenye kugusa maslahi ya nchi hizo mbili, miongoni mwao amani ya eneo na usalama, biashara na namna Afrika inavyokabiliana na ugonjwa wa Covid-19.
Bwawa la Ethiopia linalojengwa kutoka mto Nile linatarajiwa kutoa nguvu za umeme kwa raia milioni 65 wa Ethiopia.
Kwa kaisi kikubwa mno, Misri inategemea mto Nile kwa maji ya matumizi yake na hivi karibuni ilionya kwamba ujenzi wa bwawa hilo ni tishio kwa taifa lake.
Kenya ni mmoja wa waangalizi katika jopo la wapatanishi la Umoja wa Afrika katika utatuzi wa mgogoro unatokana na bwawa hilo.
Mali imemuachilia Waziri Mkuu wa zamani aliyekuwa amekamatwa
Mali imemuachilia Waziri Mkuu wa zamani aliyekuwa amekamatwa.
Mamlaka huko Mali imetangaza kuachiliwa huru kwa wanasiasa kadhaa na wanajeshi waliokamatwa wakati wa mapinduzi ya Agosti.
Walioachiliwa ni pamoja na aliyekuwa Waziri Mkuu, Boubou Cissé.
Taarifa rasmi imeonesha kwamba waliokamatwa bado watasubiri uamuzi wa mahakama ikiwa kutakuwa na haja ya kufanya hivyo.
Jumatatu, serikali ya mpito ilitangaza baraza jipya la mawaziri ambapo wanajeshi waliopanga mapinduzi walikabidhiwa nafasi muhimu serikalini ikiwemo ulinzi, usalama, utawala wa mipaka na maridhiano ya kitaifa.
Jumuiya ya Kiuchumi ya Nchi za Afrika Magharibi ECOWAS, imeiondolea Mali vikwazo, na kutambua kile ilichokitaja kama kupigwa kwa hatua muhimu kuelekea kwenye utaratibu wa kikatiba.
Nani ataingia kwenye fainali ya kuwania uongozi wa (WTO)
Wagombea watano wanaowania kuchukua uongozi wa Shirika la Biashara Duniani (WTO), wanatarajia kufahamu nani anaingia kwenye fainali ya kinyang’anyiro hicho, Alhamisi.
Kumekuwa na tetesi kwamba huenda wagombea wa Nigeria na Korea Kusini wakaingia kwenye awamu ya fainali.
Aidha Shirika la WTO halijawahi kuongozwa ama na mwanamke au mwafrika.
Wagombea wote wamekuwa na majukumu wanayoyatekeleza katika ngazi ya kidunia.
Aliyekuwa waziri wa fedha wa Nigeria Ngozi Okonjo-Iweala aliwahi kuhudumu kama Mkurugenzi mkuu wa Benki ya Dunia ilihali akiwa waziri wa fedha wa Kenya, Amina Mohamed alikuwa mwenyekiti wa mkutano wa mawaziri wa WTO katika mkutano uliofanyika Nairobi mwaka 2015.
Aidha, wawili hao wanakabiliwa na upinzani kutoka kwa waziri wa biashara wa Korea Kusini Yoo Myung-hee, pamoja na Mohammad Maziad Al-Tuwaijri mshauri wa familia ya kifalme wa Saudi Arabia na Liam Fox, aliyekuwa waziri wa Uingereza.
Matumaini ni kwamba ikiwa mwafrika ndiye atakayechaguliwa kuongoza Shirika la WTO, hilo huenda likaimarisha uchumi, ambao umekwama kwa asilimia 2 hadi 3 kwa muda katika kiwango cha wastani duniani.
Mgombea atakayeibuka na ushindi anatarajiwa kutangazwa mwezi ujao.
Joshua Cheptegei avunja rekodi ya mita 10,000
Mwanariadha wa Uganda Joshua Cheptegei alivunja rekodi ya dunia upande wa wanaume katika mbio za mita 10,000 huku mwanariadha wa Ethiopia Letesenbet Giedy akivunja rekodi ya wanawake katika mbio za mita 5000 mjini valencia nchini Uhispania.
Cheptegei mwenye umri wa miaka 24 aliweka muda wa dakika 26 na sekunde 11 na kuvunja rekodi ya miaka 15 iliowekwa na mwanariadha wa Ethiopia Kenenisa Bekele kwa zaidi ya sekunde sita.
Gidey mwenye umri wa miaka 22 aliweka muda wa dakika 14 na sekunde 6.62 na kuvunja rekodi iliowekwa na Tirunesh Dibaba 2008.
Walifikia muda huo katika mbioa za NN Valencia za rekodi za dunia.
Nafurahia alisema Gidey ambaye alishinda medali ya shaba katika mbio za mita 10,000 kwenye mashindano ya riadha ya dunia mjini Doha Qatar 2019.
‘’Hii imekuwa ndoto ya muda mrefu. Ni kitu kikubwa kwangu. Rekodi ya Bekele ya awali ya muda wa dakika 26 na sekunde 17 .53 ilisimama kwa muda mrefu bila kuvunjwa’’.
Rekodi ya awali ya Bekele ya dakika 26 na sekunde 17.53 ilikuwa ndio ya muda mrefu zaidi kudumu katika historia kwa mbio za mita 10,000 kwa wanaume.
Mafanikio ya Cheptegei yanaadhimisha rekodi ya nne duniani katika kipindi cha miezi 10, baada ya kuvunja rekodi ya mbio za marathoni ya kilomita 10 Desemba na kilomita 5 mwezi Februari.
Katika mbio za Monaco Diamond League zilizofanyika Agosti, alivunja rekodi nyingine ya dunia ya Bekele, ya miaka 16 ya mita 5,000 kwa sekunde mbili.