Na hadi hapo tumefika mwisho wa matangazo yetu ya moja kwa moja hivi leo.Hadi hapo kesho panapo majaaliwa
Wito watolewa kutambua miili iliyotolewa kutoka mtoni, Kenya
AFPCopyright: AFP
Mto Tana uko kaskazini mashariki mwa KenyaImage caption: Mto Tana uko kaskazini mashariki mwa Kenya
Kikundi cha kutetea haki za binadamu nchini Kenya
kimehimiza serikali kusaidia kutambua miili 16 iliyoopolewa kutoka Mto Tana
katika mkoa wa kaskazini mashariki katika kipindi cha miezi mitatu iliyopita.
"Baadhi
ya familia zinaweza kukosa rasilimali ya kuwasafirisha huko kwa zoezi la
utambuzi wa mwili," Hussein Khalid, mkurugenzi mtendaji wa Haki Africa,
aliambia BBC.
Alikuwa
akijibu mwito wa polisi kwa wale wanaotafuta jamaa waliopotea kutembelea chumba
cha kuhifadhi maiti katika kaunti ya Garissa.
Miili
iliyopatikana imeoza sana, wengine walikuwa wamefungwa kamba mikononi na miguuni,
wengine walikuwa wamefungwa mawe kwa kuzunguka, ripoti ya vyombo vya habari nchini
humo zimesema.
Hakuna miili
yoyote iliyokuwa na aina yoyote ya hati za kitambulisho juu yao.
Polisi
wanasema waathiriwa waliuawa na miili yao kutupwa mtoni, kituo cha runinga ya
eneo ya Citizen TV.
Familia zingine zinazotafuta jamaa wao waliopotea huku wakiwa na wasiwasi, walitembelea chumba cha kuhifadhia maiti huko Garissa Jumatatu lakini wakaondoka wakiwa wamevunjika moyo.
Sampuli kutoka kwa miili hiyo sasa imepelekwa katika maabara ya serikali kwa uchunguzi.
Wachezaji wa Judo wapigwa marufuku kushiriki Olympiki kwa kukataa kucheza na Muisraeli
GCopyright: G
Fethi Nourine alijiondoa katika michuano ya Olympiki muda mfupi kabla ya mchezo kuanzaImage caption: Fethi Nourine alijiondoa katika michuano ya Olympiki muda mfupi kabla ya mchezo kuanza
Shirikisho la
kimataifa la mchezo wa Judo (IJF) limewawekea
marufuku ya miaka 10 mchezaji wa Algerian
plapamoja na mkufunzi wake kwasbabu walijiondoa kwenye michuano ya Olympiki ili
kuepuka mechi na Muisraeli.
IJF lilisema kuwa Fethi Nourine na Amar
Benikhlef walitumia mechi za Tokyo kama
jukwa la kupinga na kuendeleza propaganda.
Mchezaji wa Algeria
alisema uungaji mkono wake kwa Wapalestina ulimfanya asiweze kushindana na
Muisraeli.
Zaidi ya 80 wafariki kutokana na mafuriko Sudan
EPACopyright: EPA
Baadhi ya nyumba za kuishi na majengo mengine yamezama ndani ya maji ya mafurikoImage caption: Baadhi ya nyumba za kuishi na majengo mengine yamezama ndani ya maji ya mafuriko
Zaidi ya watu 80 wamefariki kutokana na mafuriko nchini Sudan
tangu msimu wa mvua uipoanza mwezi Julai, maafisa wanasema.
Msemaji wa Baraza la
kitaifa la ulinzi wa raia alisema Jumatatu kuwa watu 84 wamekufa na wengine 67 walijeruhiwa.
Mvua za kubwa
iliyonyesha imeathiri takriban majimbo
14 kati ya 18 nchini humo, huku nyumba zaidi ya 30,000 zikiangamia au
kuharibika.
Mazao na miundo
mbinu ya umma pia vimeathiriwa.
Umoja wa Mataifa
unakadiria kuwa walau watu 102,000 wameathiriwa na mvua kubwa na mafuriko kote
nchini Sudan.
Mwaka jana, Sudan ilitangaza hali ya tahadhari kitaifa kwa miezi mitatu kutokana na mafuriko
ambayo yaliwauwa watu wapatao 100 na kuwaathiri wengine zaidi ya 600,000, na kuharibu zaidi ya nyuma 100,000.
Familia ya jasusi wa Somalia yakataa tume ya rais
BBCCopyright: BBC
Bi Ikran Tahlil alitoweka mwezi JuniImage caption: Bi Ikran Tahlil alitoweka mwezi Juni
Familia yaafisa wa
ujasusi wa Somalia aliyepotea, Ikran Tahlil, imeikataa tume ya uchunguzi iliyoundwa
na Rais Mohamed Abdullahi
"Farmajo" Mohamed kwa ajili ya kuchunguza kutoweka kwake mwezi Juni.
Rais Farmajo alituma
ujumbe kwenye Twitter kwamba jopo hilo la watu watano la uchunguzi lingepewa ‘’jukumu
la taasisi ya kisheria kwa ajili ya utekelezaji wa haki".
Hatahivyo, familia
ya Bi Tahlil imepinga uteuzi wa tume ya uchunguzi na wamesema kuwa wanaamini
mahakama ya kijeshi tu jeshi tu ndiyo
inayoweza kushugulikia kesi hiyo.
"Hatuna imani
na hatutaikubali tume ya uchunguzi ambayo imeteuliwa na rais kuchunguza kesi ya
Ikran. Tunaimani tu na mahakama ya
jeshi, na ndio maana tuliwasilisha kesi huko ," Qali Mohamud, mama yake Bi
Tahlil, aliiambia Universal TV.
Waziri Mkuu wa
Somalia Mohamed Hussein Roble, ambaye
ametofautiana na RaisFarmajo kuhusu kezi hiyo, bado hajasema lolote
kuhusiana na uundwaji wa tume hiyo.
Tarehe 2 Septemba,
Shirika la ujasusi na usalama nchini humo (Nisa) lilisema kuwa Bi Tahlil, ambaye
alifanya kazi katika idara yake ya usalama wa mtandao, aliuawa na al-Shabab baada ya kutekwa nyara mjini Mogadishu.
Hatahivyo, al-Shabab
ilikanusha kuhusika na kutoweka kwa Bi Tahlil na madai ya kifo chake.
R. Kelly alimdhulumu kingono Aaliyah alipokuwa na umri wa miaka 13 au 14, korti yaambiwa
Getty ImagesCopyright: Getty Images
R. Kelly alimnyanyasa kingono mwimbaji wa
zamani wa R&B marehemu Aaliyah
wakati alipokuwa na umri wa miaka 13 au 14, mmoja wa wacheza densi wake wa
zamani ameiambia korti.
Mwanamke huyo, ambaye alitoa ushahidi chini ya jina Angela, aliiambia korti kwamba alikuwa ameona nyota huyo akifanya tendo la
ngono kwa Aaliyah kwenye basi la usafiri
Tukio hilo linadaiwa kutokea mwaka mmoja kabla ya Bwana
Kelly kuoa mwimbaji huyo kinyume cha sheria, akiwa na miaka 15.
Bwana Kelly, 54, anakanusha mashtaka yote
dhidi yake.
Ni pamoja na shtaka moja la udanganyifu -
ambalo linamtaja kama mkuu kundi lenye
hila la "kuwateka wasichana na
vijana" kwa malengo ya ngono’. Ameshtakiwa pia kwa mashtaka manane ya
kukiuka sheria za kuzuia ngono kati ya
majimbo
Getty ImagesCopyright: Getty Images
Mwimbaji huyo, ambaye jina lake kamili ni Robert Kelly, hakushtakiwa kwa kubaka au kushambulia, lakini waendesha mashtaka wanaruhusiwa kutoa ushahidi wa uhalifu unaowezekana unaohusiana na mashtaka ya ujambazi, bila kujali ni lini yalitokea.
Ushuhuda wa Angela ulikuja siku ya 15 ya kesi, huko Brooklyn, New York.
Alikuwa mtu wa 10 anayetuhumu R Kelly kusimama kortini kutoa ushahidi na akasimulia kisa cha unyanyasaji wa kijinsia wa waathiriwa waliokuwa na umri mdogo .
Alisema alianza kufanya mapenzi na Bwana Kelly mnamo 1991, wakati bado alikuwa shuleni.
Kesi hiyo inaendelea
Mwanamke anayetumia maelfu ya pauni kuhakikisha njiwa wake wanapendeza kwa mitindo
Daily MailCopyright: Daily Mail
Wametengewa chumba chao kwa matumizi ya kibinafsiImage caption: Wametengewa chumba chao kwa matumizi ya kibinafsi
Huenda umewahi kusikua kuwa kuhusu watu wanaotumia pesa nyingi
sana kugarimia maisha ya mbwa wao.
Lakini mara hii
mambo sio mbwa tena. Mwanamke mmoja kwa jina amekuwa akitumia kitita cha Pauni4,000 kila mwaka kuwapendezesha njiwa wake
wawili aliowaasili ambao kwa sasa wana chumba , kabati lao la nguo na hata
kutembezwa ndani ya baiskeli ya watoto wachanga.
Meggy
Johnson, mwenye umri wa miaka 23, kutoka Lincolnshire, aliwanusuru ndege hao aina ya njiwa kwa majina
Sky na Moose, baada ya kupatikana wakiwa
wametupwa walipokuwa bado vifaranga
Daily MailCopyright: Daily Mail
Hutumia kiti hiki cha magurudumu ambacho kwa kawaida hutumiwa kwa watoto kuwatembeza njiwa wake kuwafurahishaImage caption: Hutumia kiti hiki cha magurudumu ambacho kwa kawaida hutumiwa kwa watoto kuwatembeza njiwa wake kuwafurahisha
Bi Meggy Johnson aliwatunza na kuhakikisha kuwa wanarejea katika hali nzuri ya afya kwa kuwalisha kwa mikono yake kwa kipindi cha wiki sita- na katika kipindi hiki alitokea kujenga uhusiano wa karibu nao na kuwapenda sana.
Kwa sasa, njiwa hao wanaishi “maisha ya anasa” huku wakifanyiwa sherehe za siku ya kuzaliwa, wakipewa wanasesele laini na kutembezwa.
Licha ya huduma yake ya upendo, Meggy, mara nyingi hupata kauli za matusi kutoka kwa watu wasiojulikana ambao humuita“panya wa kuruka ”,lakini anasema ni marafiki zake wazuri na “wanastahili fursa”, ya kupewa matunzo bora.
Daily MailCopyright: Daily Mail
Licha ya huduma yake ya upendo, Meggy, mara nyingi hupata kauli za matusi kutoka kwa watu wasiojulikanaImage caption: Licha ya huduma yake ya upendo, Meggy, mara nyingi hupata kauli za matusi kutoka kwa watu wasiojulikana
Mpenzi huyu wa wanyama hutumia pauni 400 kila mwezi kuwafurahisha njiwa hao pamoja na ndege wengine wawili aliowaokoa.
Met Gala 2021: Watu maarufu walivyoonyesha mavazi yao ya kifahari kwenye zulia jekundu
Getty ImagesCopyright: Getty Images
Mwanamuziki Billie Eilish, ambaye alikuwa mshereheshaji mwenza wa tukio, alifananishwa na Marilyn MonrImage caption: Mwanamuziki Billie Eilish, ambaye alikuwa mshereheshaji mwenza wa tukio, alifananishwa na Marilyn Monr
The Met Gala - ni mojawapo ya maonyesho makubwa zaidi ya mitindo ya mavazi na matukio yanayowakutanisha nyota wa fani za filamu na mitindo ya mavazi duniani. Nyota hao walipita kwenye zulia jekundu jijini New York kuonyesha na kunadi mavazi yao yaliyobuniwa na nembo kubwa za mavazi. Washiriki ni baadhi ya watu maarufu zaidi duniani.
Likifanyika kwa madhumuni ya kuchangisha pesa kwa ajili ya jumba la Makumbusho taasisi ya - Metropolitan Museum of Art's Costume Institute.
Onyesho la Gala limerejea baada ya kuahirishwa mwaka jana kutokana na janga la corona.
Hawa ni baadhi ya watu maarufu na jinsi walivyojinadi kwenye zulia jekundu:
Getty ImagesCopyright: Getty Images
Mshereheshaji mwenza wa tuki mchezaji tenisi maarufu Naomi Osaka alionyesha gauni lake la rangi za kupendeza la nembo ya Louis Vuitton na mtindo wake wa kipekee wa nywele -ambao unasemekana una asili yake ya Haiti na JapanImage caption: Mshereheshaji mwenza wa tuki mchezaji tenisi maarufu Naomi Osaka alionyesha gauni lake la rangi za kupendeza la nembo ya Louis Vuitton na mtindo wake wa kipekee wa nywele -ambao unasemekana una asili yake ya Haiti na Japan
Getty ImagesCopyright: Getty Images
Mwanamashairi Amanda Gorman, ambaye allisoma ushairi wake katika sherehe ya kuapishwa kwa Rais wa Marekani Joe Biden , alikuwa pia mshereheshaji mwenza. Alichagua kuvaa gauli lake la nembo ya Vera Wang na kitambaa cha kichwani cha channel "a re-imagined Statue of Liberty"Image caption: Mwanamashairi Amanda Gorman, ambaye allisoma ushairi wake katika sherehe ya kuapishwa kwa Rais wa Marekani Joe Biden , alikuwa pia mshereheshaji mwenza. Alichagua kuvaa gauli lake la nembo ya Vera Wang na kitambaa cha kichwani cha channel "a re-imagined Statue of Liberty"
Getty ImagesCopyright: Getty Images
Muonekano wa Kim Kardashian uliibua msururu picha za watu na vibonzo vya kuigiza vazi hili kwenye mitandao ya kijamiiImage caption: Muonekano wa Kim Kardashian uliibua msururu picha za watu na vibonzo vya kuigiza vazi hili kwenye mitandao ya kijamii
Getty ImagesCopyright: Getty Images
A$AP Rocky na mpenzi wake Rihanna waliwasili kuchelewa kimtindo, huku wakiwa wamevalia mavazi yanayoshabihianaImage caption: A$AP Rocky na mpenzi wake Rihanna waliwasili kuchelewa kimtindo, huku wakiwa wamevalia mavazi yanayoshabihiana
Getty ImagesCopyright: Getty Images
Mchezaji nyota wa tenisi Serena Williams aliwavutia wengi kwa vazi lake lililofunika mwili la nembo ya Gucci bodysuit ambalo lilishuka hadi mguuni lilinoonekana mithili ya manyoya ya ndegeImage caption: Mchezaji nyota wa tenisi Serena Williams aliwavutia wengi kwa vazi lake lililofunika mwili la nembo ya Gucci bodysuit ambalo lilishuka hadi mguuni lilinoonekana mithili ya manyoya ya ndege
Getty ImagesCopyright: Getty Images
Eilish alisindikizwa na kaka yake, Finneas O'Connell, ambaye aliamua kuchagua kuvaa suti kiatu na barakoa vya rangi nyekunduImage caption: Eilish alisindikizwa na kaka yake, Finneas O'Connell, ambaye aliamua kuchagua kuvaa suti kiatu na barakoa vya rangi nyekundu
Getty ImagesCopyright: Getty Images
Frank Ocean aliwasili kwenye tukio akiwa na mwanasesere wa robot wa rangi ya kijaniImage caption: Frank Ocean aliwasili kwenye tukio akiwa na mwanasesere wa robot wa rangi ya kijani
Getty ImagesCopyright: Getty Images
Rapper Lil Nas X kwanza aliingia na vazi hili ...ambalo lilificha vazi la suti la Versace armour ambalo baadaye alilifichuaImage caption: Rapper Lil Nas X kwanza aliingia na vazi hili ...ambalo lilificha vazi la suti la Versace armour ambalo baadaye alilifichua
Mama yake Waziri mkuu wa Uingereza Charlotte Johnson Wahl afariki
Getty ImagesCopyright: Getty Images
Waziri mkuu Boris Johnson pamoja na mama yake, Charlotte Johnson Wahl, na dada yake Rachel mwaka 2004Image caption: Waziri mkuu Boris Johnson pamoja na mama yake, Charlotte Johnson Wahl, na dada yake Rachel mwaka 2004
Mama yake Waziri
mkuu wa Uingereza Charlotte Johnson Wahl amefariki dunia akiwa
na umri wa miaka 79.
Taarifa iliyochapishwa katika gazeti la Times nchini Uingereza
inasema amefariki kifo cha "ghafla na cha amani" katika
hospitali ya St Mary magharibi mwa London.
Boris Johnson wakati mmoja
alimuelezea mama yake, ambaye alikuwa mchoraji kama mwenye "mamlaka
ya juu zaidi " katika familia.
Watu maarufu kutoka vyama vyote vya kisiasa, akiwemo
kiongozi wa chama cha Labour Sir Keir Starmer, wametuma salamu za
rambirambi kwa Bw Johnson.
Katika ujumbe wake wa Twitter Sir Keir aliandika : "Pole
sana, nimepata taarifa ya waziri mkuu kumpoteza mama yake. Natoa rambirambi kwake binafsi na kwa
familia yake."
Bi Johnson Wahl, ambaye baba yake alikuwa rais wa Tume ya Ulaya
ya haki za binadamu katika miaka ya 1970, aliolewa na Stanley Johnson mwaka 1963 kabla ya kumaliza shahada yake katika Chuo
kikuu cha Oxford kama mhitimu wa kwanza wa kike kumaliza masomo ya shahada chuoni hapo
akiwa ameolewa.
Wawili hao walikuwa na watoto wanne - Boris, mwandishi wa habari
Rachel, waziri wa zamani wa mazingira Jo na mwanamazingira Leo. Ndoa yao
ilivunjika 1979.
Kama msanii wa uchoraji, Bi Johnson Wahl alitengeneza jina lake kama
mchoraji wa picha, ambapo wasanii wa maigizo Joanna Lumley na author Jilly Cooper wakiwa miongoni mwa watu
aliowachora.
Mnamo mwaka 1988, aliolewa
na Profesa Mmarekani Nicholas Wahl na akahamia New York – ambapo alianza kuchora
michoro ya jiji. Alirejea London baada ya kifo cha mume wake mwaka 1996.
Akiwa na umri wa miaka 40, alipatwa na maradhi ya ubongo ya Parkinson,
lakini aliendelea kuchora, akitembea kwa usaidizi wa kifaa cha kutembea.
Wanawake wa Afghanistan wapinga masharti makali ya mavazi ya wanafunzi wa kike
DR BAHAR JALALICopyright: DR BAHAR JALALI
Kampeni ya mtandao wa kijamii ilianzishwa na Dkt Bahar JalaliImage caption: Kampeni ya mtandao wa kijamii ilianzishwa na Dkt Bahar Jalali
Wanawake wa Afghanistan
wameanzisha kampeni ya mtandaoni dhidi ya masharti makali ya mavazi ya
wanafunzi wa kike.
Wakitumia Hashtag ya #DoNotTouchMyClothes
na #AfghanistanCulture,wengi wanasambaza picha za nguo zao nzuri za kitamaduni.
Mwandishi wa BBC Sodaba Haidare alizungumza na mwanamke mmoja aliye kinara wa
kampeni hii.
Andika "Nguo za jadi za
Afghanistan" kwenye Google na utashangaa kwa kuona nguo za kitamaduni
zenye rangi nyingi. Kila moja ni ya kipekee, na mapambo ya mikono na muundo ,
nzito, vioo vidogo vilivyowekwa kama nakshi kwa uangalifu kifuani, sketi ndefu
na zenye kupendeza. Wanawake wengine huvaa kofia zilizopambwa, wengine huvaa
vitambaa kichwani, kulingana na mkoa gani wa Afghanistan wanatoka.
Toleo la nyuma la nguo kama
hizo lilikuwa linavaliwa kila siku na wanawake wanaokwenda chuo kikuu au mahali
pao pa kazi katika miaka 20 iliyopita.
Wakati mwingine suruali
ilibadilishwa na suruali ya jeans na vitambaa viliwekwa juu ya vichwa vyao
badala ya juu ya mabega.
EPACopyright: EPA
Wanafunzi wa kike wa Afghanistan walivaa nguo nyeusi wakati wa mkutano wa kuunga mkono Taliban aktika chuo kikuu mjini KabulImage caption: Wanafunzi wa kike wa Afghanistan walivaa nguo nyeusi wakati wa mkutano wa kuunga mkono Taliban aktika chuo kikuu mjini Kabul
Lakini picha za wanawake walio na nguo ndefu ndefu zilizofunikwa na abaya za rangi nyeusi, kufunika uso na mikono yao, na kukusanyika huko Kabul mwishoni mwa wiki kuunga mkono "agizo la Taliban" zimeonesha toafauti kubwa.
Katika video moja, wanawake wanaoongoza maandamano ya kuunga mkono Taliban katika mji mkuu walionekana wakisema wanawake wa Afghanistan wanaojipaka urembo na katika nguo za kisasa "hawamukilishi mwanamke wa Kiislamu wa Afghanistan" na "hatutaki haki za wanawake ambazo ni za kigeni na kinyume na sharia "- akimaanisha sheria ya Kiislamu inayoungwa mkono na Taliban.
Watu sita wafariki katika shambulio la kuvizia Burkina Faso
AFPCopyright: AFP
Burkina Faso imekuwa ikikabiliana na wapiganaji wa Jihad kwa miaka mingiImage caption: Burkina Faso imekuwa ikikabiliana na wapiganaji wa Jihad kwa miaka mingi
Shambulio la
kuvizia dhidi ya msafara wa maafisa wa usalama nchini Burkina Faso
uliokuwa ukisafirisha malori ya mafuta kutoka kwenye mgodi wa machimbo ya
dhahabu, karibu na mpaka wa Niger limewauwa maafisa wa usalama sita,
maafisa wanasema.
Watu saba
wamejeruhiwa baada ya kile ambacho serikali ya jimbo mashariki mwa Burkina Faso ilisema lilikuwa ni shambulio la jihadi.
Miaka miwili
iliyopita watu 39 waliuawa wakati msafara wa magari uliokuwa ukitoka eneo hilo
hilo kushambuliwa.
Tukio hilo
lilisababisha kufungwa kwa shughuli za uzalishaji kwa takriban mwaka mmoja.
Tangu mwaka 2015 mashambulio
ya makundi yenye uhusiano na Islamic
State na al-Qaeda wamewauwa zaidi ya watu 1,500 na kuwalazimisha zaidi
ya milioni moja wengine kuyahama makazi yao.
Mji wa Kigali Rwanda wanzisha usafiri wa baiskeli ili kuepusha uchafuzi wa hali ya hewa
BBCCopyright: BBC
Baiskeli za GuraRide kwa sasa zimewekwa katika maeneo 13 ya jiji la KigaliImage caption: Baiskeli za GuraRide kwa sasa zimewekwa katika maeneo 13 ya jiji la Kigali
Mji wa Kigali umeanzisha aina mpya ya kusafiri mjini humo kwa
kutumia baiskeli kama sehemuyajuhudi za
Rwandaza kukabiliana na uchafuzi wa
mazingira na kupunguza hewa ya kaboni katika miji na vituo vya miji vinavyoongezeka nchini humo.
Wasafiri wataweza kutumia baiskeli hizo kwa kupokezana katika mji
mkuu Kigali kwa bei ya chini ikilinganishwa na usafiri mwingine uliopo mjini
humo.
BBCCopyright: BBC
Kijana akienda kuchukua baiskeli kwa ajili ya kuendeshaImage caption: Kijana akienda kuchukua baiskeli kwa ajili ya kuendesha
Mjini Kigali, mtaa wa Remera baiskeli nyingi zenye rangi ya kijani na manjano zimeegeshwa katika kila kona ya barabara.
Wakazi wa mji huo wanapakua application kwenye play store ya simu zao, ili waweze kutumia baiskeli yetu’’, anaeleza kijana wa kike ambaye amekuwa akitoa maelezo kwa wapita njia wanaoashuhudia jinsi ya matumizi ya maiskeli hizo.
Kuna vituo 13 vya baiskeli hizi mjini Kigali ambako pia kuna barabara maalumu za kuendeshea baiskeli. Mtaa wa Remera karibu na uwanja wa mpira kuna vituo vingine na baadhi wameanza kutumia baiskeli hizi.
BBCCopyright: BBC
Barabara za baiskeli zimeandaliwa kando ya barabara kuuImage caption: Barabara za baiskeli zimeandaliwa kando ya barabara kuu
Kwa mjibu wa kampuni ya ‘Gura Ride’ inayosimamia mpango huu anayetaka baiskeli anaichukua katika kituo kilicho karibuna kisha shughuli zake kuiweka kwenye kituo kingine kilicho karibu na mwisho wa safari yake.
Hatahivyo changamoto iliyopo bado nikwamba bado kuna barabara chache za kuendeshea baiskeli hizi mjini kigali ,pia milima iliyopo mjini Kigali inaweza kuwa kikwazo.
BBCCopyright: BBC
Barabara ziko maeneo mawili ya jiji kwa sasaImage caption: Barabara ziko maeneo mawili ya jiji kwa sasa
Lakini wahusika wana majibu kwa changamoto hizo, Jerry Ndayishimiye ni afisa wa GuraRide:
Meya wa jiji la Kigali Pudence Rubingisa amesema lengo kubwala mradi huuni kukabiliana na uhalibifu wa mazingira:‘’tunataka usafiri unaotusaidia kulinda uchafuzi wa mazingira, kusafiri bila kutumia magari kwani tutakaposafiri kwa kutumia baiskeli itakuwafaidakubwa kwa afya zetu kwa kupata hewa safi’’
Revocant Karemangingo alipigwa risasi mita 50 kutoka kwenye makazi yake nchini MsumbijiImage caption: Revocant Karemangingo alipigwa risasi mita 50 kutoka kwenye makazi yake nchini Msumbiji
Mfanyabiashara Mnyarwanda amepigwa risasi na kuuawa katika
mainspaa ya Matola ,kilomita chache kutoka mji mkuu wa Msumbiji, Maputo.
Levocat Karemangingo
alipigwa risasi karibu mita 50 kutoka kwenye makazi yake yaliyopo katika eneo la Liberdade Jumatatu asubuhi.
Imedaiwa kuwa
uhalifu huo ulifanywa na majambazi waliokuwa katika magari matatu ambao
walilizuwia gari lake kabla ya kummiminia risasi.
Wauaji hao hadi sasa
hawajulikana, jambo lililoitikisa jamii ya Wanyarwanda wanaoishi Msumbiji.
Polisi walikuwa
kwenye eneo la tukio kufanya uchunguzi wa mwili wake na baadaye ulipelekwa
kwenye hospitali ya jimbo.
Baadhi ya
Wanyarwanda wamewaambia waandishi wa habari kuwa uhalifu huo uliwalenga raia
wanaopinga serikali ya sasa ya Rwanda na kudai kuwa watu wengi wanalengwa.
Wanyarwanda walioko
Msumbiji wameiomba serikali kuwapatia ulinzi zaidi.
Mwaka 2019, Mnyarwanda
mwingine, Louis Baziga, aliuawa kwa risasi katika kitongoji cha Maputo baada ya watu wenye gari kuzuia gari lake na kumpiga risasi.
Alifahamika kuiunga mkono serikali ya sasa ya Rwanda.
Kiungo wa
kati wa klabu ya Manchester United Paul Pogba aliisaidia klabu yake kuilaza Newcastle4-1siku ya Jumamosikabla ya
kujiunga na nyota wa muziki wa Nigeria Burna Boy kuwatumbuiza raia.
Pogba ambaye
familia yake inatoka nchini Guinea , alicheza pamoja na Cristiano Ronaldokatika uwanja wa Old Trafford huku nyota huyo
wa Ureno akifunga magoli mawili baada ya kurudi katika timu hiyo kutoka
Juventus.
Mchezaji
huyo ambaye ni mshindi mara mbili wa kombe la dunia na Ufaransa , alitoa pasi mbili
za magoli kabla ya kwenda katika tamasha la muziki la Parklife music festival mjini Manchester na kushiriki pamoja na Burna
Boy, ambaye alikuwa amevalia tishati ya Manchester United.
Habari za moja kwa moja
time_stated_uk
Na hadi hapo tumefika mwisho wa matangazo yetu ya moja kwa moja hivi leo.Hadi hapo kesho panapo majaaliwa
Wito watolewa kutambua miili iliyotolewa kutoka mtoni, Kenya
Kikundi cha kutetea haki za binadamu nchini Kenya kimehimiza serikali kusaidia kutambua miili 16 iliyoopolewa kutoka Mto Tana katika mkoa wa kaskazini mashariki katika kipindi cha miezi mitatu iliyopita.
"Baadhi ya familia zinaweza kukosa rasilimali ya kuwasafirisha huko kwa zoezi la utambuzi wa mwili," Hussein Khalid, mkurugenzi mtendaji wa Haki Africa, aliambia BBC.
Alikuwa akijibu mwito wa polisi kwa wale wanaotafuta jamaa waliopotea kutembelea chumba cha kuhifadhi maiti katika kaunti ya Garissa.
Miili iliyopatikana imeoza sana, wengine walikuwa wamefungwa kamba mikononi na miguuni, wengine walikuwa wamefungwa mawe kwa kuzunguka, ripoti ya vyombo vya habari nchini humo zimesema.
Hakuna miili yoyote iliyokuwa na aina yoyote ya hati za kitambulisho juu yao.
Polisi wanasema waathiriwa waliuawa na miili yao kutupwa mtoni, kituo cha runinga ya eneo ya Citizen TV.
Familia zingine zinazotafuta jamaa wao waliopotea huku wakiwa na wasiwasi, walitembelea chumba cha kuhifadhia maiti huko Garissa Jumatatu lakini wakaondoka wakiwa wamevunjika moyo.
Sampuli kutoka kwa miili hiyo sasa imepelekwa katika maabara ya serikali kwa uchunguzi.
Wachezaji wa Judo wapigwa marufuku kushiriki Olympiki kwa kukataa kucheza na Muisraeli
Shirikisho la kimataifa la mchezo wa Judo (IJF) limewawekea marufuku ya miaka 10 mchezaji wa Algerian plapamoja na mkufunzi wake kwasbabu walijiondoa kwenye michuano ya Olympiki ili kuepuka mechi na Muisraeli.
IJF lilisema kuwa Fethi Nourine na Amar Benikhlef walitumia mechi za Tokyo kama jukwa la kupinga na kuendeleza propaganda.
Mchezaji wa Algeria alisema uungaji mkono wake kwa Wapalestina ulimfanya asiweze kushindana na Muisraeli.
Zaidi ya 80 wafariki kutokana na mafuriko Sudan
Zaidi ya watu 80 wamefariki kutokana na mafuriko nchini Sudan tangu msimu wa mvua uipoanza mwezi Julai, maafisa wanasema.
Msemaji wa Baraza la kitaifa la ulinzi wa raia alisema Jumatatu kuwa watu 84 wamekufa na wengine 67 walijeruhiwa.
Mvua za kubwa iliyonyesha imeathiri takriban majimbo 14 kati ya 18 nchini humo, huku nyumba zaidi ya 30,000 zikiangamia au kuharibika.
Mazao na miundo mbinu ya umma pia vimeathiriwa.
Umoja wa Mataifa unakadiria kuwa walau watu 102,000 wameathiriwa na mvua kubwa na mafuriko kote nchini Sudan.
Mwaka jana, Sudan ilitangaza hali ya tahadhari kitaifa kwa miezi mitatu kutokana na mafuriko ambayo yaliwauwa watu wapatao 100 na kuwaathiri wengine zaidi ya 600,000, na kuharibu zaidi ya nyuma 100,000.
Familia ya jasusi wa Somalia yakataa tume ya rais
Familia yaafisa wa ujasusi wa Somalia aliyepotea, Ikran Tahlil, imeikataa tume ya uchunguzi iliyoundwa na Rais Mohamed Abdullahi "Farmajo" Mohamed kwa ajili ya kuchunguza kutoweka kwake mwezi Juni.
Rais Farmajo alituma ujumbe kwenye Twitter kwamba jopo hilo la watu watano la uchunguzi lingepewa ‘’jukumu la taasisi ya kisheria kwa ajili ya utekelezaji wa haki".
Hatahivyo, familia ya Bi Tahlil imepinga uteuzi wa tume ya uchunguzi na wamesema kuwa wanaamini mahakama ya kijeshi tu jeshi tu ndiyo inayoweza kushugulikia kesi hiyo.
"Hatuna imani na hatutaikubali tume ya uchunguzi ambayo imeteuliwa na rais kuchunguza kesi ya Ikran. Tunaimani tu na mahakama ya jeshi, na ndio maana tuliwasilisha kesi huko ," Qali Mohamud, mama yake Bi Tahlil, aliiambia Universal TV.
Waziri Mkuu wa Somalia Mohamed Hussein Roble, ambaye ametofautiana na RaisFarmajo kuhusu kezi hiyo, bado hajasema lolote kuhusiana na uundwaji wa tume hiyo.
Tarehe 2 Septemba, Shirika la ujasusi na usalama nchini humo (Nisa) lilisema kuwa Bi Tahlil, ambaye alifanya kazi katika idara yake ya usalama wa mtandao, aliuawa na al-Shabab baada ya kutekwa nyara mjini Mogadishu.
Hatahivyo, al-Shabab ilikanusha kuhusika na kutoweka kwa Bi Tahlil na madai ya kifo chake.
R. Kelly alimdhulumu kingono Aaliyah alipokuwa na umri wa miaka 13 au 14, korti yaambiwa
R. Kelly alimnyanyasa kingono mwimbaji wa zamani wa R&B marehemu Aaliyah wakati alipokuwa na umri wa miaka 13 au 14, mmoja wa wacheza densi wake wa zamani ameiambia korti.
Mwanamke huyo, ambaye alitoa ushahidi chini ya jina Angela, aliiambia korti kwamba alikuwa ameona nyota huyo akifanya tendo la ngono kwa Aaliyah kwenye basi la usafiri
Tukio hilo linadaiwa kutokea mwaka mmoja kabla ya Bwana Kelly kuoa mwimbaji huyo kinyume cha sheria, akiwa na miaka 15.
Bwana Kelly, 54, anakanusha mashtaka yote dhidi yake.
Ni pamoja na shtaka moja la udanganyifu - ambalo linamtaja kama mkuu kundi lenye hila la "kuwateka wasichana na vijana" kwa malengo ya ngono’. Ameshtakiwa pia kwa mashtaka manane ya kukiuka sheria za kuzuia ngono kati ya majimbo
Mwimbaji huyo, ambaye jina lake kamili ni Robert Kelly, hakushtakiwa kwa kubaka au kushambulia, lakini waendesha mashtaka wanaruhusiwa kutoa ushahidi wa uhalifu unaowezekana unaohusiana na mashtaka ya ujambazi, bila kujali ni lini yalitokea.
Ushuhuda wa Angela ulikuja siku ya 15 ya kesi, huko Brooklyn, New York.
Alikuwa mtu wa 10 anayetuhumu R Kelly kusimama kortini kutoa ushahidi na akasimulia kisa cha unyanyasaji wa kijinsia wa waathiriwa waliokuwa na umri mdogo .
Alisema alianza kufanya mapenzi na Bwana Kelly mnamo 1991, wakati bado alikuwa shuleni.
Kesi hiyo inaendelea
Mwanamke anayetumia maelfu ya pauni kuhakikisha njiwa wake wanapendeza kwa mitindo
Huenda umewahi kusikua kuwa kuhusu watu wanaotumia pesa nyingi sana kugarimia maisha ya mbwa wao.
Lakini mara hii mambo sio mbwa tena. Mwanamke mmoja kwa jina amekuwa akitumia kitita cha Pauni4,000 kila mwaka kuwapendezesha njiwa wake wawili aliowaasili ambao kwa sasa wana chumba , kabati lao la nguo na hata kutembezwa ndani ya baiskeli ya watoto wachanga.
Meggy Johnson, mwenye umri wa miaka 23, kutoka Lincolnshire, aliwanusuru ndege hao aina ya njiwa kwa majina Sky na Moose, baada ya kupatikana wakiwa wametupwa walipokuwa bado vifaranga
Bi Meggy Johnson aliwatunza na kuhakikisha kuwa wanarejea katika hali nzuri ya afya kwa kuwalisha kwa mikono yake kwa kipindi cha wiki sita- na katika kipindi hiki alitokea kujenga uhusiano wa karibu nao na kuwapenda sana.
Kwa sasa, njiwa hao wanaishi “maisha ya anasa” huku wakifanyiwa sherehe za siku ya kuzaliwa, wakipewa wanasesele laini na kutembezwa.
Licha ya huduma yake ya upendo, Meggy, mara nyingi hupata kauli za matusi kutoka kwa watu wasiojulikana ambao humuita“panya wa kuruka ”,lakini anasema ni marafiki zake wazuri na “wanastahili fursa”, ya kupewa matunzo bora.
Mpenzi huyu wa wanyama hutumia pauni 400 kila mwezi kuwafurahisha njiwa hao pamoja na ndege wengine wawili aliowaokoa.
Met Gala 2021: Watu maarufu walivyoonyesha mavazi yao ya kifahari kwenye zulia jekundu
The Met Gala - ni mojawapo ya maonyesho makubwa zaidi ya mitindo ya mavazi na matukio yanayowakutanisha nyota wa fani za filamu na mitindo ya mavazi duniani. Nyota hao walipita kwenye zulia jekundu jijini New York kuonyesha na kunadi mavazi yao yaliyobuniwa na nembo kubwa za mavazi. Washiriki ni baadhi ya watu maarufu zaidi duniani.
Likifanyika kwa madhumuni ya kuchangisha pesa kwa ajili ya jumba la Makumbusho taasisi ya - Metropolitan Museum of Art's Costume Institute.
Onyesho la Gala limerejea baada ya kuahirishwa mwaka jana kutokana na janga la corona.
Hawa ni baadhi ya watu maarufu na jinsi walivyojinadi kwenye zulia jekundu:
Mama yake Waziri mkuu wa Uingereza Charlotte Johnson Wahl afariki
Mama yake Waziri mkuu wa Uingereza Charlotte Johnson Wahl amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 79.
Taarifa iliyochapishwa katika gazeti la Times nchini Uingereza inasema amefariki kifo cha "ghafla na cha amani" katika hospitali ya St Mary magharibi mwa London.
Boris Johnson wakati mmoja alimuelezea mama yake, ambaye alikuwa mchoraji kama mwenye "mamlaka ya juu zaidi " katika familia.
Watu maarufu kutoka vyama vyote vya kisiasa, akiwemo kiongozi wa chama cha Labour Sir Keir Starmer, wametuma salamu za rambirambi kwa Bw Johnson.
Katika ujumbe wake wa Twitter Sir Keir aliandika : "Pole sana, nimepata taarifa ya waziri mkuu kumpoteza mama yake. Natoa rambirambi kwake binafsi na kwa familia yake."
Bi Johnson Wahl, ambaye baba yake alikuwa rais wa Tume ya Ulaya ya haki za binadamu katika miaka ya 1970, aliolewa na Stanley Johnson mwaka 1963 kabla ya kumaliza shahada yake katika Chuo kikuu cha Oxford kama mhitimu wa kwanza wa kike kumaliza masomo ya shahada chuoni hapo akiwa ameolewa.
Wawili hao walikuwa na watoto wanne - Boris, mwandishi wa habari Rachel, waziri wa zamani wa mazingira Jo na mwanamazingira Leo. Ndoa yao ilivunjika 1979.
Kama msanii wa uchoraji, Bi Johnson Wahl alitengeneza jina lake kama mchoraji wa picha, ambapo wasanii wa maigizo Joanna Lumley na author Jilly Cooper wakiwa miongoni mwa watu aliowachora.
Mnamo mwaka 1988, aliolewa na Profesa Mmarekani Nicholas Wahl na akahamia New York – ambapo alianza kuchora michoro ya jiji. Alirejea London baada ya kifo cha mume wake mwaka 1996.
Akiwa na umri wa miaka 40, alipatwa na maradhi ya ubongo ya Parkinson, lakini aliendelea kuchora, akitembea kwa usaidizi wa kifaa cha kutembea.
Wanawake wa Afghanistan wapinga masharti makali ya mavazi ya wanafunzi wa kike
Wanawake wa Afghanistan wameanzisha kampeni ya mtandaoni dhidi ya masharti makali ya mavazi ya wanafunzi wa kike.
Wakitumia Hashtag ya #DoNotTouchMyClothes na #AfghanistanCulture,wengi wanasambaza picha za nguo zao nzuri za kitamaduni. Mwandishi wa BBC Sodaba Haidare alizungumza na mwanamke mmoja aliye kinara wa kampeni hii.
Andika "Nguo za jadi za Afghanistan" kwenye Google na utashangaa kwa kuona nguo za kitamaduni zenye rangi nyingi. Kila moja ni ya kipekee, na mapambo ya mikono na muundo , nzito, vioo vidogo vilivyowekwa kama nakshi kwa uangalifu kifuani, sketi ndefu na zenye kupendeza. Wanawake wengine huvaa kofia zilizopambwa, wengine huvaa vitambaa kichwani, kulingana na mkoa gani wa Afghanistan wanatoka.
Toleo la nyuma la nguo kama hizo lilikuwa linavaliwa kila siku na wanawake wanaokwenda chuo kikuu au mahali pao pa kazi katika miaka 20 iliyopita.
Wakati mwingine suruali ilibadilishwa na suruali ya jeans na vitambaa viliwekwa juu ya vichwa vyao badala ya juu ya mabega.
Lakini picha za wanawake walio na nguo ndefu ndefu zilizofunikwa na abaya za rangi nyeusi, kufunika uso na mikono yao, na kukusanyika huko Kabul mwishoni mwa wiki kuunga mkono "agizo la Taliban" zimeonesha toafauti kubwa.
Katika video moja, wanawake wanaoongoza maandamano ya kuunga mkono Taliban katika mji mkuu walionekana wakisema wanawake wa Afghanistan wanaojipaka urembo na katika nguo za kisasa "hawamukilishi mwanamke wa Kiislamu wa Afghanistan" na "hatutaki haki za wanawake ambazo ni za kigeni na kinyume na sharia "- akimaanisha sheria ya Kiislamu inayoungwa mkono na Taliban.
Taarifa zaidi kuhusu wanawake Afghanistan:
Watu sita wafariki katika shambulio la kuvizia Burkina Faso
Shambulio la kuvizia dhidi ya msafara wa maafisa wa usalama nchini Burkina Faso uliokuwa ukisafirisha malori ya mafuta kutoka kwenye mgodi wa machimbo ya dhahabu, karibu na mpaka wa Niger limewauwa maafisa wa usalama sita, maafisa wanasema.
Watu saba wamejeruhiwa baada ya kile ambacho serikali ya jimbo mashariki mwa Burkina Faso ilisema lilikuwa ni shambulio la jihadi.
Miaka miwili iliyopita watu 39 waliuawa wakati msafara wa magari uliokuwa ukitoka eneo hilo hilo kushambuliwa.
Tukio hilo lilisababisha kufungwa kwa shughuli za uzalishaji kwa takriban mwaka mmoja.
Tangu mwaka 2015 mashambulio ya makundi yenye uhusiano na Islamic State na al-Qaeda wamewauwa zaidi ya watu 1,500 na kuwalazimisha zaidi ya milioni moja wengine kuyahama makazi yao.
Fahamu kundi linaloihangaisha Nigeria licha ya kuwa na jeshi kubwa
Boko Haram: Hizi ndizo sababu sita za serikali ya Nigeria kushindwa kuliangamiza kundi la kigaidi la Boko Haram
Mji wa Kigali Rwanda wanzisha usafiri wa baiskeli ili kuepusha uchafuzi wa hali ya hewa
Mji wa Kigali umeanzisha aina mpya ya kusafiri mjini humo kwa kutumia baiskeli kama sehemuyajuhudi za Rwandaza kukabiliana na uchafuzi wa mazingira na kupunguza hewa ya kaboni katika miji na vituo vya miji vinavyoongezeka nchini humo.
Wasafiri wataweza kutumia baiskeli hizo kwa kupokezana katika mji mkuu Kigali kwa bei ya chini ikilinganishwa na usafiri mwingine uliopo mjini humo.
Mjini Kigali, mtaa wa Remera baiskeli nyingi zenye rangi ya kijani na manjano zimeegeshwa katika kila kona ya barabara.
Wakazi wa mji huo wanapakua application kwenye play store ya simu zao, ili waweze kutumia baiskeli yetu’’, anaeleza kijana wa kike ambaye amekuwa akitoa maelezo kwa wapita njia wanaoashuhudia jinsi ya matumizi ya maiskeli hizo.
Kuna vituo 13 vya baiskeli hizi mjini Kigali ambako pia kuna barabara maalumu za kuendeshea baiskeli. Mtaa wa Remera karibu na uwanja wa mpira kuna vituo vingine na baadhi wameanza kutumia baiskeli hizi.
Kwa mjibu wa kampuni ya ‘Gura Ride’ inayosimamia mpango huu anayetaka baiskeli anaichukua katika kituo kilicho karibuna kisha shughuli zake kuiweka kwenye kituo kingine kilicho karibu na mwisho wa safari yake.
Hatahivyo changamoto iliyopo bado nikwamba bado kuna barabara chache za kuendeshea baiskeli hizi mjini kigali ,pia milima iliyopo mjini Kigali inaweza kuwa kikwazo.
Lakini wahusika wana majibu kwa changamoto hizo, Jerry Ndayishimiye ni afisa wa GuraRide:
Meya wa jiji la Kigali Pudence Rubingisa amesema lengo kubwala mradi huuni kukabiliana na uhalibifu wa mazingira:‘’tunataka usafiri unaotusaidia kulinda uchafuzi wa mazingira, kusafiri bila kutumia magari kwani tutakaposafiri kwa kutumia baiskeli itakuwafaidakubwa kwa afya zetu kwa kupata hewa safi’’
Fahamu miji 10 safi zaidi Afrika
Hii ni miji 5 duniani yenye gharama ya chini zaidi ya kuishi
Mfanyabiashara Mnyarwanda apigwa risasi na kuuawa Msumbiji
Mfanyabiashara Mnyarwanda amepigwa risasi na kuuawa katika mainspaa ya Matola ,kilomita chache kutoka mji mkuu wa Msumbiji, Maputo.
Levocat Karemangingo alipigwa risasi karibu mita 50 kutoka kwenye makazi yake yaliyopo katika eneo la Liberdade Jumatatu asubuhi.
Imedaiwa kuwa uhalifu huo ulifanywa na majambazi waliokuwa katika magari matatu ambao walilizuwia gari lake kabla ya kummiminia risasi.
Wauaji hao hadi sasa hawajulikana, jambo lililoitikisa jamii ya Wanyarwanda wanaoishi Msumbiji.
Polisi walikuwa kwenye eneo la tukio kufanya uchunguzi wa mwili wake na baadaye ulipelekwa kwenye hospitali ya jimbo.
Baadhi ya Wanyarwanda wamewaambia waandishi wa habari kuwa uhalifu huo uliwalenga raia wanaopinga serikali ya sasa ya Rwanda na kudai kuwa watu wengi wanalengwa.
Wanyarwanda walioko Msumbiji wameiomba serikali kuwapatia ulinzi zaidi.
Mwaka 2019, Mnyarwanda mwingine, Louis Baziga, aliuawa kwa risasi katika kitongoji cha Maputo baada ya watu wenye gari kuzuia gari lake na kumpiga risasi. Alifahamika kuiunga mkono serikali ya sasa ya Rwanda.
Taarifa zaidi kuhusu Msumbiji:
Paul Pogba na Burnaboy watumbuiza katika tamasha la muziki England
Kiungo wa kati wa klabu ya Manchester United Paul Pogba aliisaidia klabu yake kuilaza Newcastle4-1siku ya Jumamosikabla ya kujiunga na nyota wa muziki wa Nigeria Burna Boy kuwatumbuiza raia.
Pogba ambaye familia yake inatoka nchini Guinea , alicheza pamoja na Cristiano Ronaldokatika uwanja wa Old Trafford huku nyota huyo wa Ureno akifunga magoli mawili baada ya kurudi katika timu hiyo kutoka Juventus.
Mchezaji huyo ambaye ni mshindi mara mbili wa kombe la dunia na Ufaransa , alitoa pasi mbili za magoli kabla ya kwenda katika tamasha la muziki la Parklife music festival mjini Manchester na kushiriki pamoja na Burna Boy, ambaye alikuwa amevalia tishati ya Manchester United.