Fatuma zarika asema mpinzani wake atapa kipigo

Fatuma zarika asema mpinzani wake atapa kipigo

Bondia wa Kenya Fatuma Zarika anasema mpinzani wake kutoka Mexico, Yamileth Mercado, yuko mjini Nairobi kama mtalii.

Hivyo basi Fatuma anamshauri Mercado ajionee mbuga za wanyama wa pori na kufurahia mandhari safi ya jiji kuu la Kenya lakini asiwe na matumaini ya kuibuka mshindi Jumamosi ya Septemba tarehe 8 wakati Zarika atatetea ubingwa wake wa dunia wa chama cha WBC uzani wa super-bantam.