Tetesi za soka Ulaya Ijumaa tarehe 05.03.2021: Konate, Lacazette, Elmohamady, Fernandes, Koulibaly, Pereira, Jakobs

Mchezaji wa safu ya ulinzi wa timu ya RB Leipzig Mfaransa Ibrahima Konate

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha,

Mchezaji wa safu ya ulinzi wa timu ya RB Leipzig Mfaransa Ibrahima Konate

Arsenal ni miongoni mwa klabu kadhaa zinazoangalia uwezekano wa kumhamisha mchezaji wa safu ya ulinzi wa timu ya RB Leipzig Mfaransa Ibrahima Konate mweye umri wa miaka 21. (Standard).

Konate ni mmoja kati ya wachezaji sita ambao Gunners wanashugulika kuwapata, huku klabu hiyo pia ikiwa tayari kumuuza mshambuliaji wa Ufarnsa Alexandre Lacazette, 29, kwa bei inayofaa. (Football.London)

Maelezo ya picha,

Kiungo wa kati wa Manchester United Mreno Bruno Fernandes

Kiungo wa kati wa Manchester United Mreno Bruno Fernandes, 26,yuko tayari kusaini mkataba mpya ambao utaongeza mshahara wake mara dufu na kuweza kupata malipo ya takriban pauni 200,000 kwa wiki. (Sun)

Mlinzi wa Misri Ahmed Elmohamady, 33, ataondoka Aston Villa kwa mkataba usio na malipo msimu huu huku klabu hiyo ikiwa haina mipango ya kumpatia mkataba mpya. (Football Insider)

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha,

Kalidou Koulibaly

Napoli wamepunguza kiwango cha pesa walizokuwa wanadai kwa ajili ya kumuuza Kalidou Koulibaly hadi kufikia kiwango cha euro milioni 45 (£38.7m), huku Bayern Munich wakiaminiwa kuwa mbele ya Liverpool na Manchester United katika mbio za kusaini mkataba na mlinzi huyo kutoka Senegal mwenye umri wa miaka 21. (Il Mattino - in Italian)

Leicester City wamefufua haja yao kwa mchezaji ambaye wamekuwa wakimtaka kwa muda mrefu Ismail Jakobs, mwenye umri wa miaka 21, lakini the Foxes wanakabiliwa na ushindani kutoka Brighton ambao pia wanamfuatilia kwa karibu mchezaji huyo wa kimataifa kutoka klabu ya Ujerumani ya Cologne. (Mail)

Maelezo ya picha,

Kiungo wa kati Andreas Pereira

Manchester United wanatafuta klabu mbadala kwa ajili ya kiungo wa kati Andreas Pereira, 25, msimu huu kwasababu Lazio wanatarajiwa kukubali hilo na kubadilisha makataba wa Mbrazili huo kutoka mkataba wa mkopo na kusaini mkataba wa kudumu nae. (Corriere Dello Sport - in Italian)

Shinikizo la kifedha linaweza kuilazimisha klabu ya Valencia kumuuza mshambuliaji wa Ureno Goncalo Guedes, 24, ambaye analengwa na West Ham katika msimu ujao (O Jogo, via Sun)

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha,

Kiungo wa safu ya kati wa Chelsea Jorginho

Juventus wamemtaja kiungo wa safu ya kati wa Chelsea Jorginho, 29, kama chaguo lao la pili iwapo watashindwa kusaini mkataba na Muitalia Manuel Locatelli, 23, kutoka klabu ya Sassuolo. (Calciomercato - in Italian)

Wakati huo huo, Mlinzi Juventus anayeskwa na timu mbali mbali Radu Dragusin mwenye umri wa miaka 19- raia wa Romania ambaye awali alihusishwa na taarifa za kuhamia Crystal Palace, yuko tayari kusaini mkataba mpya na klabu ya Turin. (Goal)

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha,

Winga wa Real Madrid na Uhispania Lucas Vazquez

Leeds United wanakabiliwa na ushindani kutoka AC Milan katika kujaribu kusaini mkataba na winga wa Real Madrid na Uhispania Lucas Vazquez, 29, ambaye mlkataba wake katika klabu ya Bernabeu unamalizika msimu ujao.(Fichajes, via Sport Witness)

Eintracht Frankfurt wamesema kuwa hawatamzuia mkurugenzi wao wa mchezo Fredi Bobic, 49,kama atachagua kuondoka, huku Manchester United, West Ham na Hertha Berlin wakihusishwa na taaruifa za kumnunua Mjerumani huyo. (Bild, via Team Talk)

Chelsea itatia kibindoni asilimia isiyojulikana ya ada itakayopokewa na Brighton wakimuuza Lamptey baada klabu hizo mbili kukubaliana katika mpango ambao ulimwezesha mlinzi huyo kuondoka Stamford Bridge na kutua Seagulls Januari 2020. (Express)

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha,

Mshambuliaji wa Manchester City na Argentina Sergio Aguero

Mgombea uraisi wa Barcelona Joan Laporta anataka mshambuliaji wa Manchester City na Argentina Sergio Aguero, 32, kujiunga na klabu hiyo msimu huu. (Mail)

Mkufunzi wa Gunners Mikel Arteta amesema "umakini kabisa" kuongoza Arsenal licha ya madai yanayomhusisha Barcelona - lakini mazungumzo ya mkataba mpya utakaomwezesha kusalia Emirates hayajaanza. (ESPN)

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha,

Mshambuliaji wa Ufaransa Alexandre Lacazette

Arteta anasema mazungumzo kuhusu kandarasi ya mshambuliaji wa Ufaransa Alexandre Lacazette,29, ambaye mkataba wake wa sasa na Arsenal unaendelea hadi 2023, yataanza hivi "karibuni". (Mail)

Winga wa zamani wa England Ashley Young, 35, anamatumaini ya kunyakua taji la Serie, Inter Milan kabla ya kurejea klabu katika yake ya kwanza ya Watford kwa mkataba wa bila malipo msimu huu. (Mirror)

Maelezo ya picha,

Meneja wa Liverpool Meneja Jurgen Klopp

Meneja Jurgen Klopp amekiri kuwa Liverpool itakuwa na wakati mgumu kuwavutia wachezaji endapo haitafuzu kujiunga na Ligi ya Mabingwa. (Goal)

Mkurugenzi wa AC Milan Frederic Massara amefichua kuwa klabu hiyo bado haijaamua ikiwa itaanzisha mazungumzo ya kumnunua Fikayo Tomori,23, - lakini AC Milan inasisitiza bei ya £26m iliyotolewa na Chelsea iko juu sana. (Express)

Maelezo ya picha,

Mkufunzi wa Manchester United, Ole Gunnar Solskjaer

Mkufunzi wa Manchester United, Ole Gunnar Solskjaer ameonya juu ya kiwango cha pesa ambacho kitatumiwa na klabu hiyo msimu huu wa joto wakati Old inapojiandaa kutangaza matokeo yao ya kifedha ya hivi karibuni . (Times - subscription required)