Hamad alikuwa amekata tamaa, baada ya moja ya jamii nchini Kuwaiti imekuwa ikinyimwa haki ya uraia
Soma ZaidiHaki za Kibinadamu
Kenya yaamuriwa kuwalipa fidia waathiriwa unyanyasaji wa kingono
Copyright: Getty ImagesImage caption: Karibu watu 1,000 waliuawa katika ghasia hizo Mahakama Kuu nchini Kenya ameamuru serikali kuwalipa fidia ya karibu $30,000 watu wanne kwa kushindwa kuwapatia ulinzi dhidi ya unyanyasaji wa kingono na kijinsia wakati wa ghasia za baada ya uchaguzi zilizokumba nchi hiyo baada ya uchaguzi wa mwaka 2007-2008.
Uamuzi huo unaonekana kuwamkubwa, huku Naitore Nyamu-Mathenge – mkuu wa madaktari wa kundi la kutetea haki za binadamu akiunga mkono hatua hiyo ya mahakama-akisema hatiamye haki imetekelezwa.
Hata hivyo ametoa wito kwa serikali kuongeza juhudi za kuzuia vitendo kama hivyo kutokea tena siku zijazo.
Akitua hukumu hiyo Jaji Weldon Korir alisema manusura hao wana haki ya kuishi maisha na kwamba walinyanyaswa wakati waliposhambuliwa.
Pia aliongeza kuwa serikali ilishindwa kuwalinda dhidi ya mateso, unyama na udhalilishaji waliyofanyiwa.
Shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch linakadiria kuwa watu 1,000 waliuawa na wengine zaidi ya 500,000 kufurushwa makwao.
Pia kulikuwa na ripoti kadhaa za ubakaji na mateso.
Ghasia zilizuka baada ya Mwai Kibaki- rais wa wakati huo kutangazwa mshindi wa uchaguzi. Mpinzani wake Raila Odinga alisema kura zimeibwa.
Rais wa sasa Uhuru Kenyatta – ambaye alimuunga mkono Bwana Kibaki – na naibu wake William Ruto – ambaye alimuunga mkono Bwana. Odinga – walishtakiwa katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu wa jinai, ICC kwa kosa la uhalifu dhidi ya binadamu baada ya kutuhumiwa kwa kuchochea ghasia.
Video content
Video caption: Mpiga picha aliye na jicho moja aeleza safari yake ya kujikwamua kimaisha Mpiga picha aliye na jicho moja aeleza safari yake ya kujikwamua kimaisha
Watu 50 wauawa katika maandamano Guinea
Copyright: Getty ImagesImage caption: Vikosi vya uslama vyalaumiwa kwa kutekeleza mauaji Guinea Shirika la kutetea haki la Amnesty International limesema karibu watu 50 wameuawa kwa kupigwa risasi katika maandamano ya kupinga serikali nchini Guinea mwaka jana.
Ripoti mpya ya shirika hilo limelaumu vikosi vya usalama kwa kutekeleza mauaji ya kiholela.
Baadhi ya waandamanaji walipigwa risasi wakiandamana dhidi ya hatua ya Rais Alpha Condé kutaka kusalia madarakani kwa muhula wa tatu.
Ripoti hiyo pia imeangazia jinsi watu 200 walivyojeruhiwa na wengine 70 kuzuiliwa kinyume cha sheria.
Uchaguzi wa urais utafanyika nchi humo baadaye mwezi Oktoba.