Serikali ya Uingereza imetoa tahadhari kwa raia wa nchi hiyo wanaosafiri kuelekea nchini Tanzania juu ya ''uwezekano'' wa kuwepo Ebola katika taifa hilo la Mashariki mwa Afrika.
Shirika la afya duniani limelalamikia ukosefu wa ushirkiano kamili kutoka serikali ya Tanzania katika utoaji taarifa kuhusu visa vinavyoshukiwa kuwa vya Ebola nchini.